Ruka hadi kwenye maudhui makuu

VIZAZI VYA KUKU

NAPENDA KUTOA UFAFANUZI WA HILI SWALA

Katika mnyororo wa vizazi vya kuku na wanyama wengine huwa kuna rank tangu kwa mababu mpaka kwa wajukuu.

Leo naomba nielezee kuhusu

Parental Stock,
F1
F2

Parental Stock/wazazi

Hawa ni kuku ambao vifaranga wao hupatikana kutaka kwa Grand parents/mabibi na mababu...

Parental stock maranyingi huwa kwenye makampuni yanayo jihusisha na BREEDING au Breeders kwa jina jingine.

Hawa maranyingi vifaranga wao huagiza nje, nchi tofauti kwa kutegemea aina ya kuku ambao wana wazalisha


F1 First filial generation

Hawa na vifaranga au kuku ambao wanazaliwa kutoka kwa kuku wazazi Parental stock huu ni uzao wa awali kabisa kutoka kwa kuku wazazi ambao huwa na Jogoo wa rangi Fulani na tetea wa rangi Fulani.

 Mfano Vifaranga F1 wa kuku Hyline pure, jogoo mzazi huwa rangi ya Grey na Tetea huwa rangi nyeupe

Ila kifaranga anaezalishwa Tetea huwa rangi Grey na jogoo huwa mweupe.

Vifaranga F1 huwa na sifa bora za ukuaji kwa wale wanyama na za utagaji kwa wale wa mayai.


F2 Second filial generation

Huu ni kizaazi cha pili, na hutokana na mayai yanayo tagwa na kizazi cha kwanza yani F1 hawa pia huwa na ubora ila hushuka viwango vya ukuaji ukilinganisha na wale waliototolewa kutoka kwa wazazi( Parental Stock)

Nimeona niliweke wazi hilo kwenu ili maswali kwangu kuhusu vifaranga yapungue...

Wengi wamekua wakitangaza kuuza F1 siwezi kukanusha kwakua sijui wapi wanazalishia Ila kama mnunuzi unayo fursa ya kuulizawapi hawa wazazi au asili ya wazazi wa hao kuku wanatokea

NB Ningumu kutambua vizazi vya kuku kwa kuangalia tu kwa macho, historia ya kuku kwa mzalishaji ndo inaweza kukupa ukweli kama ni F1 au F2 nk.

By KAHISE MTAALAMU WA KUKU

0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...