Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BIOSECURITY/ VIUMBE HAI SALAMA

ULINZI WA VIUMBE HAI /KUKU DHIDI YA MAGONJWA

Magonjwa ya kuku imekua fimbo kubwa sana kwa mfugaji hali inayopelekea kuongezeka kwa garama za kununua madawa....vifo vya kuku kuongezeka...kuku kupoteza uzito na thamani katika soko....kuteketea kwa mitaji ya wafugaji na hata kukata tamaa ya kuendelea kufuga.

Kwa kutambua hilo yafuatayo unaweza kuyatumia yakakusaidia kwa kiasi kikubwa sana kupunguza magonjwa ya kuku bandani

Moja hakikisha mradi wa kuku unakua na usimamizi mzuri muda wote kutoka kwa mtunzanzi wa kuku hasa kuwaangalia kuku wako Mara kwa Mara na kubaini changamoto zao

Mbili hakikisha banda lako limejengwa katika ubora unaostahili kwa kuzingatia uwepo wa wavu nusu ukuta na tofali au material yoyote ya kujengea nusu ukuta 0.5-0.7 m

Tatu hakikisha umejiwekea sheria za kuzifuata kwaajili ya kuwalinda kuku wako...mfano kuwepo mabuti ya kuingia nayo bandani pekee...ziwepo nguo maalumu za kuingia nazo bandani...vifaa vya kuku visihamishwe kutoka banda moja kwenda jingine......

Mhudumu wa kuku anapaswa kuanza kuwahudumia kuku wadogo kwanza ndipo aende kuwahudumia kuku wakubwa

Usifuge kuku kwa kuchanganya na ndege wengine kama BATA ,KANGA , NJIWA

Hakikisha mfumo wako wa ulishaji na unyweshaji kuku ni mzuri unao muwezesha kuku kupata maji masafi muda wrote

Hakikisha kuna dawa za kuulia wadudu mlangoni za kukanyaga kama FARM GUARD kuua vimelea pindi utokapo na unapoingia bandani

Banda la kuku linapaswa kusafishwa kwa dawa za kuua wadudu kama V-RID au TH4..nakupumzishwa kwa muda usiopungua siku 14 kisha uingize kuku wengine

Kuku wanatakiwa kupewa kinga za magonjwa yote ya virusi ili kuwafanya wawe na kings imara ya magonjwa

Epuka kuchanganya chakula cha kuku kwa kutumia pumba zilizo vunda au dagaa waliovunda,,utapunguza magonjwa

Zuia uwezavyo watu wasio na ulazima kuingia bandani...mfano watu kuja kuwatazama kuku wako mara kwa Mara...kila mnunuzi kumwingiza bandani kuangalia kuku kila wakati hupelekea magonjwa kutoka shamba moja kwenda jingine

Pale uonapo dalili ya kuku kuumwa watenge...kisha utafute usaidizi wa madaktari kugundua ni ugonjwa upi unawapata kuku na uwape Tiba kwa kumaliza dozi....usipendelee kubadilisha dawa za kuku kablaa dozi haijaisha huwapa usugu wa kupambana na magonjwa

Kama unashamba kubwa magari...au pikipiki zinazoingia kwenye shamba zipuliziwe dawa za kuua vimelea wa magonjwa

Hakikisha banda lako linakua kavu muda wote hii itapunguza saana magonjwa kama coccidiosis ambayo husumbua na kuua kuku wengi kwa wafugaji..

Kwa vifaranga hakikisha wanapata joto lakutosha wiki 2 za kwanza....pia wapewe chakula chenye ubora unaotakiwa

Mabanda yako yajengwe kitaalamu kufuata uelekeo wa upepo...pia kuangalia JUA...EAST -WEST...direction

Hakikisha vyomba utakavyo kua ukivitumia ni visafi na maji utakayo kua ukiyatumia ni salama kwa matumizi ya kuku

HIZO NI BAADHI TU YA TARATIBU ZA MUHIMU KWAAJILI YA KUZUIA MAGONJWA KWA KUKU

Imeandaliwa na GREYSON KAHISE mtaalamu wa kuku

Simu 0769799728/0653387629

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...