Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UTUNZAJI RANDA BANDANI



MATUNZO YA RANDA
Kwetu Tanzania zipo aina kubwa mbili za randa au matandazo ya kuku ambazo zimekua zikitumika
Randa za mbao
Pumba za mpunga.
Kwa kuku wa umri wowote (kifaranga na wakubwa) ni muhimu sana kuwawekea randa

Kwanini uweke randa bandani
Kwanza kabisa randa husaidia kuwepo na joto bandani, ( kuzuia baridi ya sakafu kuwafikia kuku ) hivo maginjwa kama Brooder pneumonia yanapungua.
Randa husaidia kufyonza unyevu ,maji ya kinyesi na maji yanayo mwagika bandani
Randa husaidia  kupunguza uwezekano wa kuku kupata matatizo ya miguu( Bumble foot ) inayo pelekea kuku kuvimba kwenye makanyagio na kuchechemea ( hasa jogoo).
Randa huwapa kuku rehemu salama ya malazi pia kufanya tabia yao ya asili kuparua parua kama (kuoga flani )
Randa hutumika kuwekwa kwenye viota ambamo kuku atakua akitaga hivo hupunguza (mayai kuchafuka na kupasuka )


UTATUNZAJE RANDA
Hakikisha maji hayamwagiki juu ya randa mengi, na pindi yatakapo mwagika randa mbichi itolewe nje kuzuia ueneaji wa ubichi bandani.
Geuza randa Mara nyingi uwezavyo (Falking) kuruhusu randa mbichi kukauka.
Hakikisha randa imesambazwa kwa usawa kusiwe na milima na mabonde bandani.

Napenda elimu hii iwafikie wafugaji wengi zaidi TANZANIA  unaweza kushare kwenyw groups nyingine za ufugaji kuku

Jipatie
Kitabu cha ufugaji kuku 10000
Formula ya kuku rika zote 20000
Andiko la mradi wa kuku (bei ni kutokana na ukubwa wa mradi)
Wasiliana nami kwa ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

Mr GREYSON KAHISE Mtaalamu wa kuku
instagram~ @kuku ni biashara  tz
Facebook~ Ufugaji kibiashara
whatsApp 0769799728 0653387629
Call๐Ÿ“ž 0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji ๐Ÿ‘‰Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. ๐Ÿ‘†Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. ๐Ÿ‘‰ Chakula ๐Ÿ‘†Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. ๐Ÿ‘Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo ๐Ÿ‘‰Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja ๐Ÿ‘‰Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili ๐Ÿ‘‰Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...