Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JENGA BANDA BORA LA KUKU

NYUMBA YA KUISHI KUKU/POULTRY HOUSE


Kwanini nimeamua kuita nyumba ya kuishi kuku/poultry house. Sababu ni kwamba sehemu kuku anapoishi panatakiwa kuwa na vigezo vyote stahiki, ili kumpa kuku uhusu wa kuishi, na kumkinga dhidi ya magonjwa na wanyama wengine hatari kwake.

Nyumba ya kuku inatakiwa kuwa na vitu viuatavyo

👉 Paa
Liezekwe kwa Bati, nyasi, Trubai au kitu chochote kitakacho zuia maji, miale ya jua , ndege kuingia bandani.

👉Sakafu
Iwe imara na rahisi kusafishika, kwa kutegemea uwezo na aina ya banda Sakafu pendekezwa ni ile yenye Rough Cement ili kuruhusu unyevu kufyonzwa, pia unaweza jenga na kupaka (udongo wa kichuguu) maeneo ya vijijini.

👉Madirisha
Yajengwe mapana, kwa wavu kuruhusu upepo kuingia na kutoka, hii hisaidia kuondolewa kwa hewa zisizotakiwa kama Ammonia Gas.
👆Madirisha yanatakiwa kuwepo pande kuu 2 za banda *(Pande ndefu/ ubavuni* ).
👆Nyavu zinaweza kushikiliwa kwa mbao, miti migumu au kukajengwa tofali course nyembamba kulingana na ramani ya Banda lako.

👉 Ukuta
Banda la kuku linatakiwa kuanza kwa kizuizi cha upepo kuwafikia kuku moja kwa moja wawapo kwenye sakafu, inaweza kujengwa kwa Tofali, Mbao au Bati..na Kimo cha ukuta wa Banda kinatofautiana kutokana na sehemu, Hali ya hewa(joto au baridi) na vipindi vya mvua kwa sehemu husika.

Mambo ya kuzingatia wakati wa kujenga nyumba ya kuku.

👇Nyumba inatakiwa ijengwe kuta ndogo zielekezwe uelekeo wa mashariki kwenda magaribi( East- West direction ). Na pande ndefu zielekezwe kwa kupishana na uelekeo wa upepo.
👉Nyumba iwe na nafasi ya kuwatosha kuku wote kwa kulingana na aina ya kuku wako.
👉Iruhusu mzunguko wa hewa, yani kuingia na kutoka kwa hewa
👉Isijengwe karibu na majengo ya mifugo mingine mfn Nguruwe, Ng'ombe, mbuzi.
👉Ni vema nyumba ya kulelea vifaranga ijengwe kabla ya nyumba za kuku wakubwa au kama ni nyumba moja hutumika basi hakikisha (Upepo unavuma kutoka kwa kuku wadogo kwenda kwa kuku wakubwa )
👉Iwalinde kuku dhidi ya wadudu na wanyama hatari kama vicheche, mbwa n.k.
👉Iwe imara kuzuia kuanguka, au ajali zozote zisizo za lazima kwa kuku
👉Ijengwe karibu na chanzo cha maji ya kutumia kuku wako
👉Iwe rahisi kufikiwa , pindi unaleta chakula , au huduma zozote za msingi kwa kuku.
👉Iwe karibu na stoo ya kuhifadhia chakula cha kuku.
👉Iwe na vitagio/viota vya kutagia kuku (viwekwe pindi kuku anapokaribia kutaga wiki 5-6 kabla ya kuanza kutaga)
👉Sehemu za mazoezi kwa kuku (perches) ngazi/vichanya vya kulalia au kupumzikia kuku.

👈Iwe na huduma zote za msingi kama , vyombo vya maji, vyanzo vya mwanga

 MENGINEYO
👇Isafishwe kwa dawa kabla na baada ya kuondolewa kuku
👇Iwe na sehemu ya kuweka maji ya kukanyaga yenye dawa
👇Iwe na komeo za kufungia milango
👇Iwe na mwangalizi wa karibu

KARIBU NITAFUTE NISIMAMIE UJENZI WA BANDA LAKO BORA LA KUKU LENYE VIGEZO KWA GHARAMA NAFUU SANA .

Imeandaliwa na
LGreyson Kahise
Mtaalamu wa kuku
0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...