Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA JUU YA UPATIKANAJI WA SOKO LA KUKU NA MAZAO YATOKANAYO NA KUKU


Kanuni bora za ufugaji wa kuku | East Africa Television
Kutokana na malalamiko ya wafugaji wengi wa kuku kuhusu ukosefu wa soko la uhakika la kuku na mazao yake kama nyama na mayai, yafuatayo yanapaswa kufanyika

Kabla ya kuanza mradi mfugaji anatakiwa afanye uchunguzi wa soko la atakacho zalisha

Kwanza ajue mazingira yanayo mzunguka au atakapo fugia yanahitaji nini, je ni nyama au mayai kama ni mayai je ni aina gani ya chotara au kienyeji au ya kisasa ndipo aamue kuanza uzalishaji

Kama sio hivo mfugaji ajue kama soko lake litakua mbali ni vipi atasafirisha na kutunza bidhaa zake atakazo zalisha akizingatia inabidi apate faida

Upatikanaji wa malighafi atakazo tumia wakati wa uzalishaji, ziwe ni kwa gharama ya kawaida

Anapaswa ajue wapi hasa na nani atakua mteja wake mkuu na atapambana vipi na changamoto zisizozuilika

SULUHISHO

Kuteka soko ni lazima mfugaji azalishe bidhaa yenye ubora wa hali ya juu, kama ni nyama iwe yenye sifa zote kwa mlaji na kama ni mayai yawe mazuri (Makubwa, yenye kiini cha njano, masafi, gamba lenye mvuto).

Mfugaji anapaswa kuwa mbunifu wa jinsi ya kuliteka soko la mahali alipo mfano asogeze huduma kwa mteja kumletea mayai au nyama pale anapo patikana mteja, kama ni nyama aiandae kabisa kupunguza usumbufu kwa mteja, labla mteja akichukua trey 20 apate tray moja bure.

Kwa ufugaji kama broiler unaweza kufuga kwa kutegea misimu mfano sikukuu za kitaifa, za kidini, au sherehe mbalimbali unajua tarehe mfani kuna tukio flani unakadiria lini uanze ufugaji ili soko lisikupite

Kutokana na mazingira mfugaji alipo, mnaweza kuanzisha kama umoja kama Mkoa, wilaya, kata,tarafa ambapo mtakua mnakutana na kuunganisha nguvu ya kusafirisha na uuzaji wa bidhaa zenu.

Kuendelea kufumbua macho zaidi sehemu mbali mbali kujifunza ni kwa namna gani wanapata masoko

Pia mradi ukikua mnaweza kuanzisha vituo vya kuuzia bidhaa zenu mikoani na hiyo itasaidia mtambulike kama wauzaji wa bidhaa husika.

Imeandaliwa na Mr Greyson kahise ...

mtaalamu wa kuku kwa kukusanya maoni ya wafugaji na wataalamu wa biashara 0769799728 0769799728

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...