Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MATUNZO YA KUKU


Groups za kuku ni biashara zinatoa huduma muda wowote na saa yoyote kwa urahisi na ufasaha mkubwa wengi wamesha nipa mrejesho chanya kwa mafunzo tunayotoa NAJIVUNIA HILO


Naskitika kwamba wanagroups wengine wamekua wavivu wa kusoma msg za kwenye group pindi atakapo kuta zimekua nyingi ..NAKUPA POLE... kwasababu yapo mambo ambayo yanaweza kukupata yanakua yameulizwa na yamejibiwa JITAHIDI KUSOMA USIWE MVIVU.

✔✔✔✔✔✔✔✔
 MANAGEMENT/MATUNZO YA KUKU

Chanzo kikubwa cha magonjwa au kufanya kuku kuwa na maendeleo mazuri no UCHAFU/USAFI

Kama ilivo kwa binadamu kuku wanatakiwa kuishi maisha mazuri tens sehemu safi na itakayo wafanya wawe na amani na Uhuru wa kuishi kutokana na asili yao


 ZINGATIA HAYA KWA LEO

📍Hakikisha banda lako ni safi na kavu muda wote na pindi banda likiloana badilisha matandazo kwa wakati
📍Hakikisha joto bandani hasa kwa vifaranga lipo kama inavotakiwa kwa siku elekezi kutokana na mkoa na majira ya mwaka
📍Hakikisha kuku wako wanakula chakula na kupata maji ya kutosha kutokana na idadi na aina ya kuku ulionao kwa kuzingatia umri wao
📍Hakikisha mzunguko wa hewa bandani unakua wakutosha kuruhusu hewa safi ya oksijeni ipatinane kwa urahisi, banda lenye hewa safi uligungue kwa kujiridhisha kuwa hata wew unaweza kukaa bandani kwa zaidi ya saa 1 bila kupata shida
📍Kamwe usimwage mbolea au matandazo yaliyochafuka karibu na banda lakuku
📍Usichanganye kuku na viumbe wengine au ndege wengine
📍Zuia uingiaji wa watu bandani bila sababu za msingi
📍Wachunguze kuku wako marakwamara kuona kama kuna mabadiliko yoyote ya Tabia na kiafya na uchukue hatua mapema usisubiri kuku wadhulike ndo uanze kutafuta dawa
📍Nunua vifaranga kutoka shamba linaloaminika kuwa halitakua chanzo cha magonjwa kwenye shamba lako wakati wote
📍Jifunze kuweka kumbukumbu kwa maandishi kiwango cha chakula,kuku uliopokea,kuku wanaotaga na kuku waliokufa ili iwe rahisi kujua maendeleo ya mradi wako

📍Usiwe bahili kwa kuogopa kumuita mtaalamu unaemwamini bandani japo Mara chache utajifunza mengi sahihi kuhusu ugugaji
📍Kwa Leo naona hayo yanawafaa ukizingatia hayo 90% ya changamoto za ufugaji utaziepuka

 Greyson kahise
 Mtaalamu wa kuku
 Admin save nambaangu
 0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...