Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MINYOO KWA KUKU

MAKALA KUHUSU MINYOO KWA KUKU

Minyoo ni viumbe hai ambao huishi kwa kutegemea uwepo wa kiumbe mwingine kwa malazi na chakula

Kwa kuku minyoo ipo ya aina nyingi, ipo ile ya duara, ipo ile inayokua mirefu sana ambayo ikiwapata kuku kupotea huchukua muda mrefu

CHANZO CHA MINYOO

Kuku kula chakula kichafu hasa kilicho changanyika na kinyesi...hapa hasa kama unachanganya kuku wakubwa na wadogo madhara huwa endelevu bandani usipokinga

Kuku wanao zunguka nje, kunywa maji yaliyotuama au maji yaliyokaa kwa muda mrefu pia kuparua mabaki yenye mazalia au mayai ya minyoo

Kwa kawaida minyoo huwa na mzunguko wao kunzia YAI, LAVA, PUPA ,NA MNYOO mnyoo mkubwa...hivyo minyoo ikiingia kwa kuku huvhukua muda wa wiki zaidi ya mbili kukua kufikia mnyoo kamili

Kuku akishapata minyoo wakubwa...hapa ndipo tatizo huanzia kwani mahai hutagwa kwa wingi na hutolewa kwa njia ya kinyesi na kuwafikia kuku wengine hivyo kama hatua za maksudi hazitachukuliwa ndani ya muda wa wiki 4 tangu minyoo kuingia bandani asilimia kubwa ya kuku watakua na minyoo

KUZUIA

Hakikisha mazingira yako ni salama na safi muda wote yasiyo na maji yenye kutuama kwa wala matope yanayo kuwepo kwa muda wote kuzunguka mahali kuku wanapoishi

TIBA

Kitaalamu zipo dawa nyingi za minyoo ambazo kwa ratiba iliyo zoeleka hutakiwa kutolewa na kurudiwa kila baada ya miezi mitatu

Tatizo limekuja ni upi wakati sahihi wa kuanza dozi ya minyoo...SIJAFANYA UTAFITI....ila kwa kuuliza madaktari bobezi wa kuku wanashauri dawa za awali za minyoo zitolewe baada ya miezi miwili

INASHAURIWA KWA SEHEMU ZENYE MAJI YASIYO SALAMA SANA

Na mfumo wa utoaji dawa za mjnyoo kwa Mara ya kwanza unatakiwa uwe wa kurudia kila baada ya wiki 2 rudia Mara tatu

KWA NINI IRUDIWE UNAPOANZA DOZI

Dawa za minyoo hishambulia hatua mbili za ukuaji wa minyoo..ambazo ni minyoo wakubwa na wale wanaofuata kwa ukubwa ilaa haziathiri hatua za mayai na LAVA...hivyo ukiwapa dawa kwa kurudia kila baada ya wiki mbili  Mara  3 mfululizo hii itapelekea hata yale mayai yatakua yamegeuka na kuwa minyoo wakubwa hivyo dawa itawaua na kupunguza tatizo kwa 75-85%

Ila ukiwa unasubiri kuwapa kila baada ya miezi mitatu bila kufanya hizo hatua nilizolekeza utakua unapunguza idadi ya minyoo na wakati mwingine minyoo itazidi na haitasikia dawa

Zipo dawa aina nyingi za minyoo kama Ant worms ...Piperezine...Albendazole ...zipo nyingi sana madukani



KWA URAHISI

Awamu ya kwanza ya kuwapa dawa

Baada ya miezi miwili....dozi siku 1-2

Rudia baada ya wiki 2 dozi siku 1-2

Rudia baada ya wiki 2 dozi siku 1-2

Ukimaliza hapo sasa wape dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu kuku wako watakua salama na huru dhidi ya minyoo

ZINGATIA

▶maji safi
▶chakula safi
▶banda safi
▶na fuata ratiba sahihi ya dawa hasa kila baada ya miezi mitatu zingatia usipitishe na uzipuuze

BILA SHAKA TUMEELEWANA

 Greyson kahise
 Mtaalamu wa kuku
 0769799728

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...