Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MUHIMU WAKATI WA KUCHANGANYA CJAKULA

ZINGATIA YAFUATAYO PINDI UTUMIAPO FORMULA YOYOTE YA KUCHANGANYIA CHAKULA.

Kama ifahamikavyo chakula huchukua karibu 75% ya gharama ya uzalishaji kwa kuku, hivyo wafugaji wengi wamekua wakikimbilia kupata formula ya kuchanganyia chakula.

Yafuatayo yazingatiwe
👉Pata formula ya chakula sahihi, kwa mtu mzoefu( mfugaji), mzalishaji wa chakula, wataalamu, au formula iliyo thibitishwa ubora wake practically ( usigoogle formula ukaanza kulisha kuku wako ).

👉Chagua material/ malighafi za kuchanganyia chakula, safi na kavu zisizo na uvundo.

👉Simamia upimaji wa malighafi muda na wakati wa kuchanganyiwa mfn: Unaweza kwenda mashineni ukasema uwekewe soya kg 20 ukawekewa kg 15 bila kujua, hii itaathiri moja kwa moja ubora wa Formula uwe makini.

👉Usifanye marekebisho ya Formula uliyopewa bila kuwasialiana na mtu aliekupa formula, Mabadiliko yoyote yanaharibu ubora wa formula kulingana na viwango alivyo kuwa ameweka mtengenezaji wa formula mfn: Umeambiwa uweke Premix nusu kilo wewe ukaweka robo kilo.


👉Epuka kubadilisha formula za chakula kwa kuku hao hao Mara kwa Mara

👉Simamia na hakikisha ulishaji wa kuku unafanyika kwa usahihi kulingana na maelekezo ya aliekupatia formula au chakula.

👉Pindi uonapo uzalishaji wa kuku haukupi matokeo kwa wakati wasiliana na aliekupa formula mapema, ili kama kuna marekebisho yafanyike kabla kuku hawajafikia umri mkubwa

👉Hakikisha unafuata ratiba au muda sahihi wa mwanga kwa kuku

Karibu upate
FORMULA YA LAYERS, CHATARA 20000

na KITABU CHA FUGA KUKU KITAALAMU 10000

👇Imeandaliwa na
 👉Greyson Kahise
👈Mtaalamu wa kuku
 👆0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...