Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHAKULA MBADALA

UOTESHAJI WA MAJANI HYDROPONICS FODDER

Hydroponics ni majani au mboga mboga zinazooteshwa kwa muda mfupi...hapa naongelea majani au nafaka za kulishia mifugo

HATUA ZA KUFUATA

Unachukua aina yoyote ya nafaka mfano. Mtama, mahindi au uwele

Unaosha nafaka utakayo amua kutumia kwa jiki kama inapatikana

Baada ya hapoo unayatoa kwenye maji uliyokuwa unasafisha hizoo nafaka

Unaloweka nafaka uliyoisafisha kwa maji safi kwa muda wa masaa 12

Baada ya masaa 12 nafaka yako itakuwa imeshapata maji ya kutosha

Unaziweka nafaka zako kwenye chombo ambacho kinapatikana sana sana wanatumia trey maalum za kuwekea ambazo zipo kama sahani au sinia

unazifunika kwa nylon yoyote lakini sana sana wengi wanatumia gazeti au nylon nyeusi

Unaziweka kwenye chumba ambacho hakipitishi mwanga kwa muda wa masaa 48

Baada ya masaa 48 ukienda kufunua utakuta nafaka uliyochagua imeota nyuzi nyuzi nyeupe

utatakiwa utoe trey za hiyo nafaka uliyochagua na kuweka sehemu iliyotengenezwa rasmi kama kichanja

 tray zina beba gram 200-500...na kuendelea inategemeana na ukubwa

Utatakiwa uwe unamwagilia maji kila maraa ziwe na unyevu

Baada ya siku nne kuanzia ile siku uliyoweka kwenye kichanja utatakiwa uwape kuku wako kwasababu itakuwa tayari

 Kwa ajili ya matumizi na baada ya siku saba unaweza kuwapa wanyama wengine kama sungura, ng'ombe, mbuzi, nguruwe

Majani haya huweza kupunguza kwa kiasi matumizi ya chakula pia huwa ni muhimu kwa kuongeza vitamin kwa kuku na kupelekea afya bora.

NB HAKIKISHA TREY ZAKO ZIMEOSHWA NA KUFANYIWA DISINFECTION/OSHA KWA MAJI YALIYO CHEMKA

Kuzuia Moulds na Fangasi

By KAHISE MTAALAMU WA KUKU NA SARAPIA

0769799728/0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...