Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAELEKEZO MUHIMU SANA

MAFUNZO MBALI MBALI RAHISI NA HALISI KWA MFUGAJI

 ULISHAJI
👉Lisha kuku muda mmoja kila siku, usibadilishe badilishe ratiba
👉Usibadilishe badilishe chakula
👉Usiwapunje wala kuzidisha chakula
👉Wawekee vyombo vya kutosha
👉Maji yawepo muda wote
👉Vyombo vya maji visafishwe kila siku

 UOKOTAJI WA MAYAI
 👉Panga ratiba maalumu ya kuokota mayai, mfn SAA 7:30/Am, saa 10:30 Am, saa 1:30 Pm, saa 4:30 Pm, funga report.
👉Safisha viota vya kuku, kuondoa vinyesi kila asubuhi na ongeza matandazo mayai yasipasuke
👉Okota mayai na yaweke kwenye Trey upande uliochongoka utazame chini, na upande butu uwe juu
👉Weka mayai sehemu salama isiyo na joto jingi
👉Mayai ya kutotolesha yahifadhiwe kwa siku zisizo zidi 10

 UHIFADHI WA KUMBUKUMBU
👉Hakikisha umeweka kumbukumbu zote za msingi shambani kwako kama
👆Aina ya kuku
👉Siku ya kuingia bandani
👉Idadi yao na wanaokufa
👉Gharama za chakula
👉Gharama nyingine zote
👉Mauzo
🐣Piga hesabu mapato na matumizi, hii itakusaidia kujua na kutathmini kama mtaji unakupa faida au unajiendesha kwa hasara.

 BIOSECURITY/VIUMBE HAI SALAMA
👉Usichanganye kuku na mifugo wengine
👉Usiruhusu kila mtu kuingia bandani
👉Mavazi maalumu na buti maalumu za bandani
👉Panya na ndege wazuiwe kuingia bandani uwezavyo
👉Kuku wachanjwe kwa wakati
👉Kuku waliokufa waondolewe bandani kwa wakati

JIONGEZE KITAALUMA
👉Wapeleke watunzaji kuku semina za ufugaji
👉Kama mmiliki hudhuria warsha na maonesho kujifunza ufugaji
👉Uwe mfuatiliaji wa mradi wako Mara kwa Mara
👉Ajiri /tafuta mtaalamu kuwa anaangalia mradi wako
👉Lipa vizuri wafanyakazi wako🐣

UPANUZI WA MRADI
👉Tafuta wateja wapya kila wiki
👉Imarisha uaminifu kwa wateja wazamani
👉Hakikisha bidhaa haiishi bandani, kama itaisha tafuta namna ya kumuwezesha mteja kupata bidhaa , ukikosea wanakimbia.
👉Panua mradi pindi gharama za uanzishaji zinapo rejea, usisubirie mpaka kuku wazeeke

MUHIMU
👉Ukihitaji uzalishaji bora usiogope kugharamia wataalamu
👉Pata miongozo tofauti ya ufugaji kupanua uelewa

BY
KAHISE MTAALAMU WA KUKU.
0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...