Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAELEKEZO MUHIMU SANA

MAFUNZO MBALI MBALI RAHISI NA HALISI KWA MFUGAJI

 ULISHAJI
👉Lisha kuku muda mmoja kila siku, usibadilishe badilishe ratiba
👉Usibadilishe badilishe chakula
👉Usiwapunje wala kuzidisha chakula
👉Wawekee vyombo vya kutosha
👉Maji yawepo muda wote
👉Vyombo vya maji visafishwe kila siku

 UOKOTAJI WA MAYAI
 👉Panga ratiba maalumu ya kuokota mayai, mfn SAA 7:30/Am, saa 10:30 Am, saa 1:30 Pm, saa 4:30 Pm, funga report.
👉Safisha viota vya kuku, kuondoa vinyesi kila asubuhi na ongeza matandazo mayai yasipasuke
👉Okota mayai na yaweke kwenye Trey upande uliochongoka utazame chini, na upande butu uwe juu
👉Weka mayai sehemu salama isiyo na joto jingi
👉Mayai ya kutotolesha yahifadhiwe kwa siku zisizo zidi 10

 UHIFADHI WA KUMBUKUMBU
👉Hakikisha umeweka kumbukumbu zote za msingi shambani kwako kama
👆Aina ya kuku
👉Siku ya kuingia bandani
👉Idadi yao na wanaokufa
👉Gharama za chakula
👉Gharama nyingine zote
👉Mauzo
🐣Piga hesabu mapato na matumizi, hii itakusaidia kujua na kutathmini kama mtaji unakupa faida au unajiendesha kwa hasara.

 BIOSECURITY/VIUMBE HAI SALAMA
👉Usichanganye kuku na mifugo wengine
👉Usiruhusu kila mtu kuingia bandani
👉Mavazi maalumu na buti maalumu za bandani
👉Panya na ndege wazuiwe kuingia bandani uwezavyo
👉Kuku wachanjwe kwa wakati
👉Kuku waliokufa waondolewe bandani kwa wakati

JIONGEZE KITAALUMA
👉Wapeleke watunzaji kuku semina za ufugaji
👉Kama mmiliki hudhuria warsha na maonesho kujifunza ufugaji
👉Uwe mfuatiliaji wa mradi wako Mara kwa Mara
👉Ajiri /tafuta mtaalamu kuwa anaangalia mradi wako
👉Lipa vizuri wafanyakazi wako🐣

UPANUZI WA MRADI
👉Tafuta wateja wapya kila wiki
👉Imarisha uaminifu kwa wateja wazamani
👉Hakikisha bidhaa haiishi bandani, kama itaisha tafuta namna ya kumuwezesha mteja kupata bidhaa , ukikosea wanakimbia.
👉Panua mradi pindi gharama za uanzishaji zinapo rejea, usisubirie mpaka kuku wazeeke

MUHIMU
👉Ukihitaji uzalishaji bora usiogope kugharamia wataalamu
👉Pata miongozo tofauti ya ufugaji kupanua uelewa

BY
KAHISE MTAALAMU WA KUKU.
0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...