Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUKU WA MAYAI

KUKU WA MAYAI KWA KIFUPI

Hawa ni kuku ambao vinasaba vyao huwawezesha kutaga mayai mengi kwa muda watakao fugwa

Zipo aina nyingi za kuku wa mayai hapa nitataja baadhi

Hy-line, Isa brown, Bavon brown, Lohman brown, Rhode Island n.k

Idadi ya kuku kwa mita moja mraba 7-8 ndio inayo shauriwa sana

Wanahitaji vyombo vya kutosha vya maji

Vyombo vya chakula na maji

Belly drinker 1 kuku 60-80

Chicken /feeder drinker kubwa Lita 20 kuku 50-60

Chicken  drinker/feeder ndogo lita 10 kuku 20-25
Hii huwezesha kuku kupata maji ya kutosha

NB : Kuku anatakiwa kunywa maji zaidi ya Mara mbili ya chakula anachokula kwakua zaidi ya 75% ya yai ni maji, ukipunguza maji wanapunguza kutaga ZINGATIA.

Kuku wapewe chakula kwa ratiba sahihi iliyo zoeleka usibadilishe ratiba utawastress na wataounguza kutaga

Mfano huwa unalisha saa 12 AM na 4PM hakikisha unawalisha kila Siku muda huo

Kuku walishwe kwa mfumo wa gramu ili kuzuia kujaza mafuta au kutumia chakula kingi kuzalisha yai 1., kwa kawaida kuku mmoja wa mayai anatakiwa kukupa mayai 6-7.( Hyline)


Kuku wana pitia stage 3

Brooding wakiwa vifaranga mpaka wiki 4,

Growing wiki 5 -17 na Production baada ya kuanza kutaga mayai

Hivi vipindi vinatofautiana kiuangalizi na kipindi cha kutaga hutegemea vipindi hivi( Brooding au malezi ya vifaranga na Growing)

Brooding zingatia
Chakula, Joto, hewa safi, Mwanga, nafasi ya kukaa inashauriwa 40 chicks kwa 1m2( vifaranga 40-60 kwa mita 1 mraba)

Growing
Zingatia chakula, Mwanga , nafasi na Hewa safi kwakua hapa ndo kuku anakua anaandaa mfumo mzima wa mayai

Wape kuku
Starter kwa wiki 6/8

Grower 7/8-17 au watakapo anza kutaga

Layers mash baada ya kuokota yai nakuendelea

Kuku wakianza kutaga nivema ukawapa masaa 16 ya Mwanga kama somo la mwanga linavoelekeza.

Hawa kuku wapewe chanjo zote

Siku ya 7na 21 Newcastle (ya maji au matone)
Siku ya 14na 28 gumboro( Ya maji)
Siku ya 30ndui(Ya bawa)
Kila baada ya miezi 3 rudia chanjo ya Newcastle
Wape dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu.

Uza mayai na uweke akiba kwaajili ya kuingiza kuku wengine , tunashauri uingize kuku kwa kutofautisha rika hii itakusaidia kukuza mradi pia kuwawezesha wateja wako kupata huduma muda wote.

Imeandaliwa na
GREYSON KAHISE
MTAALAMU WA KUKU
0769799728
NUNUA KITABU CHA FUGA KUKU KITAALAMU KIMEELEZEA VEMA ZAIDI.  10000.

 Nawapenda sana wafugaji

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...