Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHANJO ZA KUKU

MAKALA JUU YA
CHANJO ZA KUKU WA AINA ZOTE.

Kuna aina tofauti za magonjwa kama MAGONJWA YA VIRUSI MAGONJWA YA BAKTERIA NA MAGONJWA YA KUPE/VIROBOTO/MINYOO.

MAGONJWA YA VIRUSI KWA KUKU NI KAMA

IBDauGUMBORO

MAREX

INFECTIOUS CORTYZA/MAFUA MAKALI

FOWL POX/NDUI

ILT ..INFECTIONS LARYNGOTRACHEITIS

NEWCASTLE/KIDELI

Magonjwa haya yasababishwayo na virusi HAYATIBIKI hivyo mfugaji ni vema ukawachanja kuku wako kwa moja ya mifumo ifuatayo....

 CHANJO KIPINDI TU KUKU AKIWA

AMETOTOLEWA DAY OLD CHICK//HATCHERY ACHANJWE

Chanjo ya Mareks kwa kuku wa mayai...(l(SASSO ..KLOIRER...PURE LAYERS....BREEDER

ISIPOKUA PURE BROILERS))

Chanjo ya IBD/Gumboro

Chanjo NEWCASTLE/KIDELI

 *MFUMO WA KWANZA*

SIKU YA KUMI CHANJO YA KIDELI/ND

SIKU YA 18 CHANJO YA GUMBORO/IBD

SIKU YA 28 CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE

SIKU YA 30 CHANJO YA NDUI/FOWL POX

KILA BAADA YA MIEZI MITATU AU WIKI 9 WAPE CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE HADI PALE UTAKAPO WATOA KUKU WAKO..

MFUMO WA PILI

SIKU YA SABA CHANJO YA KIDELI/NEWCASTLE

SIKU YA 14 CHANJO YA GUMBORO/IBD

SIKU YA 21 CHANJO YA NEWCASTLE//KIDELI

SIKU YA 30 CHANJO YA NDUI/FOWL POX

KILA BAADA YA MIEZI MITATI RUDIA CHANJO YA NEWCASTLE MPAKA UTAKAPO WATOA KUKU

NB+ Majina ya chanjo husika utajifunza kwa wauzaji wa madawa wanazijua hizo chanjo vizuri

VITU VYA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHANJA KUKU

==Siku ya kuchanja kuku hakikisha kuku wametolewa maji asubuhi kabisa//uwanyime maji kwa Massaa 3au4

==Vyombo vyako vya kuwekea chanjo vioshwe vizuri kwa maji safi.

==Maji ya kuwekea chanjo yawe masafi na yachanganywe na Coper au chlorex blue ili kuondoa chlorine ya kwenye maji kufanya chanjo iwe na nguvu.

==Chanjo iliyotunzwa kwenye friji ichanganywe kwenye maji kutokana na uwingi wa kuku::Mara nyingi kopo moja la chanjo ni kwa kuku 500 dozi ndogo na 1000 dozi kubwa kwahio angalia unakuku wangapi alafu wachanganyie maji watakayo weza kumaliza.


==Wape maji yenye chanjo kwa muda wa saa1 hadi masaa2 alafu toa maji yenye chanjo.

==Dakika 5 baada ya kuweka chanjo angalia kama kuku wote//vifaranga wote wamekunywa maji yenye chanjo  kwa kutazama midomo yao itakua na rangi ya yale maji yenye copper.

==Kama kuna kifaranga hajanywa maji yachanjo mnyweshe kwa kijiko,,,au syrynge(bomba la sindano).

Chanjo ya ndui huchomwa kwa sindano kwenye bawa nivema umuite mtaalamu akuelekeze

BROILERS HAWACHANJWI FOWL POX/Ndui

HII NDIO MAKALA JUU YA RATIBA SAHIHI YA CHANJO

 IMEANDALIWA NA GREYSON KAHISEMTAALAMU WA UFUGAJI WA KUKU 0769799728 kwa maelezo na mawasiliano zaidi.


Maoni