Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS

Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji

👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti.

👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo.

👉 Chakula
👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula.

👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo
👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja

👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili

👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili

NB: Zipo shuhuda kwamba broiler 100 wanaweza kutumia mifuko minne pekee mpaka kuuza, hii inategemea sana aina ya vyakula na nafasi yao bandani.

👆Wafugaji wengi wamekua mbali na kulisha chakula wanawapa vitamin , mollases na Booster kama ifuatavyo
👉Neoxychick &multivitamin siku 1-5
👉Vitamin kama Amintoto siku ya 7-10
👉Bro-booster na Mollases siku ya 11-24
👉Avipunch booster siku zilizo salia mpaka kuuza

👉👈 Matumizi hayo ya vitamin sio sheria , kutumika ili kupunguza gharama.

👆 CHANJO
Kwa uzoefu wangu  mfumo ambao nimezoea kuutumia
👉Siku ya 7 newcastle/kideri
👉Siku ya 14 Gumboro
👉Siku ya 21 Newcastle

Mfumo B
👉Newcastle siku ya 7
👉Gumboro siku ya 14
👉Gumboro siku ya 21

NB: Ndui haichanjwi kwa broiler, ila kwa wakati mwingine wamekua wakipata ndui iwapo watachelewa kuuzwa

NAFASI
👆Kitaalamu broilers 10 wanafaa kukaa kwenye mita moja mraba, hii itasaidia sana kupunguza case za broiler kuchafuka kwa kulowesha maranda.

👆Kiasili broiler wanakunywa sana maji, hii hupelekea banda kuloana sana, hali hii imepelekea wafugaji wengi kuwa na kawaida ya kubadilisha randa Mara kwa Mara

👈Kubadili randa mara kwa Mara kwa mtazamo si sawa, ila unaweza ukawa unatoa palipo lowana sana na kubadilisha na randa kavu, hii itakusaidia sana kupunguza ugonjwa wa Mafua.

👆👉Nashauri kama itakua lazima sana basi randa zibadilishwe Mara 3 pekee IKIBIDI

👉👆👈 MASOKO
👉Broiler wamekua wakiuzwa sana , kwa mtu mmoja mmoja, familia, supermarket, wauzaji wa nyama mitaani, mahoteli, mashule na sehemu kadha wa kadha NASHAURI tafuta soko lako la uhakika na uwe tayali kulilinda bei za broiler zinatofautiana mkoa kwa mkoa.

👆👉👆 MFUMO WA UGUGAJI
👉Ili kuhakikisha soko lako linakua lakudumu na kuepuka kupoteza wateja nashauri

👆Kama una mtaji ya kuku 500, nivema ukaingiza kuku 250 wiki hili, kisha 250 baada ya wiki 2 hii itarahisisha mzunguko wa pesa ya mradi, USIFUGE  Kuku 500 kisha ukakaanao siku 30 ukiuza ndo uweke wengine itakua ngumu sana kukuza mradi (kutokana na research ndogo niliyofanya pindi nawatembelea wafugaji).

👆Kama nyama nyingine nyeupe, broilers pia wanasaidia kuimarisha afya ya malaji, ila mfugaji jitahidi kuto tumia kiwango kikubwa cha madawa ambayo yanaweza yakamdhuru mtumiaji wa mwisho

MAGONJWA KWA BROILER
👉Coccidiosis, kuhara ugoro au damu (dawa Agracox, vetacoxy, au Anticox kwa wanaohara damu)

👉Mafua , wahi mapema kubaini na unaweza kutumia ( Fluban, Flutan, Tylodox, na Enrovet)

Dawa hizi unapowapa wape na vitamin kupunguza stress kwao

IMEANDALIWA NA
👉Greyson Kahise
Mtaalamu wa kuku
0769799727 0715894582

Nakaribisha maoni zaidi kutoka kwenu na wataalamu wengine, huo ni mwongozo kwa mujibu wangu KAHISE.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...