Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MWONGOZO WA MANUNUZI YA KUKU NA UCHANGANYAJI WAO KWENYE KUKU WENYEJI.

MWONGOZO WA MANUNUZI YA KUKU NA UCHANGANYAJI WAO KWENYE KUKU WENYEJI.~ ufugaji wa kuku kitaalamu

1: Fuatilia kujua historia ya hao kuku hasa katika vipengele vifuatavyo
-Chanjo
-Magonjwa
-Uzalishaji
-Ukuaji

Hii itakupa mwanga wa kupata kuku bora au kukupa picha halisi ya nini uwafanyie kuku wako Mara baada ya kuwapata na kabla ya kuchanganya na kuku wenyeji.

2: Unatakiwa kuandaa sehemu maalumu, au chumba maalumu kwaajili ya kupokelea hao kuku wageni na kuwatenga kwa muda kabla ya kuwachanganya na wenzao. Hii itakusaidia kupunguza uwezekano wa kuleta maambukizi moja kwa moja kutoka kwa kuku wageni kwenda kwa kuku wenyeji

 FANYA YAFUATAYO
👉Wapokee kuku wako kwenye chumba maalumu
👉Wape antibiotic kuwatibu kama walikuja na vimelea wowote Tumia broad spectrum (OTC)
👉Baada ya wiki 1 wapewe chanjo ya muhimu zaidi hasa Newcastle
👉Zoezi la kuwatibu kuku kabla ya kuwachanganya lichukue angalau wiki 2
👉Changanya kuku wako wageni na kuku wenyeji( hatua ya mwisho)
👉Ukichanganya kuku ongeza vyombo vya maji na  chakula

3: Epuka kufanya zoezi la manunuzi ya kuku na kuchanganya na wengine bila kufuata utaratibu sahihi kuepusha kuku kuugua , hali itakayo kupatia shida ya kuongeza gharama ya magonjwa.

4: Wafugaji kuna kosa 1 linafanyika sana maeneo mengi.
👉Hamuoni umuhimu wa kuwatumia wataalamu, kuwasaidia mpatapo shida shambani, hii imekua ikipelekea Matibabu yanayopelekea USUGU

Nashauri ni bora uwatumie wataalamu, kwa ghrama nafuu kuliko kuanza kutibu kuku kwa muda mrefu na vifo vingi shambani.

5: Binafsi nashauri mfugaji uandae mazingira bora ya kulelea vifaranga , na ukishaandaa anza na KUFUGA KIFARANGA kuna faida nyingi zaidi kwakua utawatengeneza kuku bora ambao hawatakusumbua KULIKO kununua kuku wakubwa (mtazamo wangu kwa uzoefu).

Mwisho niwatie moyo kwamba ukifuata miongozo sahihi ya ufugaji kuku utapata matokeo chanya kabisa na utabakia kupambana na Upatikanaji wa soko la mayai au vifaranga.

Pata kitabu cha FUGA KUKU KITAALAMU BY GREYSON KAHISE kwa 10000 Tanzania Nzima.

 Imeandaliwa na
Greyson Kahise
Mtaalamu wa kuku
 0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...