Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TYPHOID /SALMONELOSIS

SALMONELA!!!!Typhoid

Leo nizungumzie kuhusu huu ugonjwa sumbufu sana kwa wafugaji wengi na usiokua na huruma kwa wengi.

Salmonella/typhoid/homa ya matumbo

Huu ni ugonjwa unao wapata kuku wa rika zote kwa nyakati tofauti na umri tofauti,

Ugonjwa huu huweza kuambukizwa kutoka kwa kuku mzazi kwenda kwenye yai na kupelekea kifaranga atakae zaliwa kuwa na ugonjwa huo (Pollourm)

 NINI VYANZO HASA
Mazingira yasiyo safi wanapoishi kuku

Chakula chenye uchafu, uvundo au chenye vinyesi vya panya.

Maji machafu au vyombo visivyo safi vya kuku.

Kutoka kwa kuku wazazi

Matumizi ya viambata visivyo kqushwa vizuri mfano Dagaa waliovunda, Damu iliyotoka kwa mfugo anaeumwa typhoid, magamba na mifupa isiyo salama( Chanzo cha uhakika cha malighafi )

Stoo yenye mpangilio mbaya , matundu yanayo ruhusu panya kuingia bandani.

 DALILI
Kuganda kwa kinyesi nyuma kilicho loana na cha rangi( Polurm kwa vifaranga)

Kinyesi cheupe kama chokaa , au wakati mwingine kinyesi mchanganyiko bandani.

Vifo visivyo koma, mfn leo1 kesho 2,,, vifo haviachi kutokea bandani ila hawafi kuku wengi sana kwa pamoja.

Kuku hupoteza uzito kwa kiwango kikubwa (mfupa wa kifuani huwa umechongoka sana)

Kuku wanaotaga kupunguza kutaga au kuacha kabisa kutaga( huathiri mfumo wa utengenezaji yai pia )

 SULUHISHO

Chakula kisafi

Mazingira safi ya banda

Mpangilio wa stoo kuzuia Panya

Nunua mayai au vifaranga kutoka kwenye shamba salama lisilo na ugonjwa.

Vyakula unavyo wapa kuku kama DAMU, DAGAA,UDUVI, MIFUPA, KONOKONO viwe vimekauka na vihifadhiwe sehemu salama isiyo na unyevu.

Watenge kuku wanaoonekana kuumwa au unaweza Fanya maamuzi magumu ya kuwauza kuku wote (SIO LAZIMA ITEGEMEE UKUBWA WA MTAJI WAKO)

Baadhi ya dawa zinazo saidia kutibu Typhoid
Trisul
Trimafarm
Esb3
Ganadexel
Enrovet
Limoxin

Ila kabla ya kujinunulia dawa wasiliana na Daktari alie karibu yako kubaini kama kweli unatibu TYPHOID/SALMONELLA.

Kwa kifupi typhoid ikiingia bandani haiponi ikatoka moja kwa moja vimelea wanakuwepo bado jitahidi sana USAFI
Maoni juu ya kupambana na PANYA

Kwangua majani mita 2-3 kuzunguka banda au Fensi kuzuia panya kuingia bandani

Zungusha mitego bandani amgalau kila baada ya mita 10 uwepo mtego wenye dawa

Ziba mianya ya kuingia panya bandani

Pangilia vizuri chakula stoo


Kwa masomo zaidi pata kitabu cha FUGA KUKU KITAALAMU ujifunze zaidi

Mikoa yote 10000 pekee.

0769799728/0715894582.

 IMEANDALIWA NA GREYSON KAHISE

MTAALAMU WA KUKU

Maoni