Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TYPHOID /SALMONELOSIS

SALMONELA!!!!Typhoid

Leo nizungumzie kuhusu huu ugonjwa sumbufu sana kwa wafugaji wengi na usiokua na huruma kwa wengi.

Salmonella/typhoid/homa ya matumbo

Huu ni ugonjwa unao wapata kuku wa rika zote kwa nyakati tofauti na umri tofauti,

Ugonjwa huu huweza kuambukizwa kutoka kwa kuku mzazi kwenda kwenye yai na kupelekea kifaranga atakae zaliwa kuwa na ugonjwa huo (Pollourm)

 NINI VYANZO HASA
Mazingira yasiyo safi wanapoishi kuku

Chakula chenye uchafu, uvundo au chenye vinyesi vya panya.

Maji machafu au vyombo visivyo safi vya kuku.

Kutoka kwa kuku wazazi

Matumizi ya viambata visivyo kqushwa vizuri mfano Dagaa waliovunda, Damu iliyotoka kwa mfugo anaeumwa typhoid, magamba na mifupa isiyo salama( Chanzo cha uhakika cha malighafi )

Stoo yenye mpangilio mbaya , matundu yanayo ruhusu panya kuingia bandani.

 DALILI
Kuganda kwa kinyesi nyuma kilicho loana na cha rangi( Polurm kwa vifaranga)

Kinyesi cheupe kama chokaa , au wakati mwingine kinyesi mchanganyiko bandani.

Vifo visivyo koma, mfn leo1 kesho 2,,, vifo haviachi kutokea bandani ila hawafi kuku wengi sana kwa pamoja.

Kuku hupoteza uzito kwa kiwango kikubwa (mfupa wa kifuani huwa umechongoka sana)

Kuku wanaotaga kupunguza kutaga au kuacha kabisa kutaga( huathiri mfumo wa utengenezaji yai pia )

 SULUHISHO

Chakula kisafi

Mazingira safi ya banda

Mpangilio wa stoo kuzuia Panya

Nunua mayai au vifaranga kutoka kwenye shamba salama lisilo na ugonjwa.

Vyakula unavyo wapa kuku kama DAMU, DAGAA,UDUVI, MIFUPA, KONOKONO viwe vimekauka na vihifadhiwe sehemu salama isiyo na unyevu.

Watenge kuku wanaoonekana kuumwa au unaweza Fanya maamuzi magumu ya kuwauza kuku wote (SIO LAZIMA ITEGEMEE UKUBWA WA MTAJI WAKO)

Baadhi ya dawa zinazo saidia kutibu Typhoid
Trisul
Trimafarm
Esb3
Ganadexel
Enrovet
Limoxin

Ila kabla ya kujinunulia dawa wasiliana na Daktari alie karibu yako kubaini kama kweli unatibu TYPHOID/SALMONELLA.

Kwa kifupi typhoid ikiingia bandani haiponi ikatoka moja kwa moja vimelea wanakuwepo bado jitahidi sana USAFI
Maoni juu ya kupambana na PANYA

Kwangua majani mita 2-3 kuzunguka banda au Fensi kuzuia panya kuingia bandani

Zungusha mitego bandani amgalau kila baada ya mita 10 uwepo mtego wenye dawa

Ziba mianya ya kuingia panya bandani

Pangilia vizuri chakula stoo


Kwa masomo zaidi pata kitabu cha FUGA KUKU KITAALAMU ujifunze zaidi

Mikoa yote 10000 pekee.

0769799728/0715894582.

 IMEANDALIWA NA GREYSON KAHISE

MTAALAMU WA KUKU

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...