Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TYPHOID /SALMONELOSIS

SALMONELA!!!!Typhoid

Leo nizungumzie kuhusu huu ugonjwa sumbufu sana kwa wafugaji wengi na usiokua na huruma kwa wengi.

Salmonella/typhoid/homa ya matumbo

Huu ni ugonjwa unao wapata kuku wa rika zote kwa nyakati tofauti na umri tofauti,

Ugonjwa huu huweza kuambukizwa kutoka kwa kuku mzazi kwenda kwenye yai na kupelekea kifaranga atakae zaliwa kuwa na ugonjwa huo (Pollourm)

 NINI VYANZO HASA
Mazingira yasiyo safi wanapoishi kuku

Chakula chenye uchafu, uvundo au chenye vinyesi vya panya.

Maji machafu au vyombo visivyo safi vya kuku.

Kutoka kwa kuku wazazi

Matumizi ya viambata visivyo kqushwa vizuri mfano Dagaa waliovunda, Damu iliyotoka kwa mfugo anaeumwa typhoid, magamba na mifupa isiyo salama( Chanzo cha uhakika cha malighafi )

Stoo yenye mpangilio mbaya , matundu yanayo ruhusu panya kuingia bandani.

 DALILI
Kuganda kwa kinyesi nyuma kilicho loana na cha rangi( Polurm kwa vifaranga)

Kinyesi cheupe kama chokaa , au wakati mwingine kinyesi mchanganyiko bandani.

Vifo visivyo koma, mfn leo1 kesho 2,,, vifo haviachi kutokea bandani ila hawafi kuku wengi sana kwa pamoja.

Kuku hupoteza uzito kwa kiwango kikubwa (mfupa wa kifuani huwa umechongoka sana)

Kuku wanaotaga kupunguza kutaga au kuacha kabisa kutaga( huathiri mfumo wa utengenezaji yai pia )

 SULUHISHO

Chakula kisafi

Mazingira safi ya banda

Mpangilio wa stoo kuzuia Panya

Nunua mayai au vifaranga kutoka kwenye shamba salama lisilo na ugonjwa.

Vyakula unavyo wapa kuku kama DAMU, DAGAA,UDUVI, MIFUPA, KONOKONO viwe vimekauka na vihifadhiwe sehemu salama isiyo na unyevu.

Watenge kuku wanaoonekana kuumwa au unaweza Fanya maamuzi magumu ya kuwauza kuku wote (SIO LAZIMA ITEGEMEE UKUBWA WA MTAJI WAKO)

Baadhi ya dawa zinazo saidia kutibu Typhoid
Trisul
Trimafarm
Esb3
Ganadexel
Enrovet
Limoxin

Ila kabla ya kujinunulia dawa wasiliana na Daktari alie karibu yako kubaini kama kweli unatibu TYPHOID/SALMONELLA.

Kwa kifupi typhoid ikiingia bandani haiponi ikatoka moja kwa moja vimelea wanakuwepo bado jitahidi sana USAFI
Maoni juu ya kupambana na PANYA

Kwangua majani mita 2-3 kuzunguka banda au Fensi kuzuia panya kuingia bandani

Zungusha mitego bandani amgalau kila baada ya mita 10 uwepo mtego wenye dawa

Ziba mianya ya kuingia panya bandani

Pangilia vizuri chakula stoo


Kwa masomo zaidi pata kitabu cha FUGA KUKU KITAALAMU ujifunze zaidi

Mikoa yote 10000 pekee.

0769799728/0715894582.

 IMEANDALIWA NA GREYSON KAHISE

MTAALAMU WA KUKU

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...