Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAMBO YA KUFANYA BANDANI

ZINGATIA YAFUATAYO KWA UFUGAJI SAHIHI.

Kama mtaalamu nimeona vema nikuletee mwongozo au utaratibu ambao utakupatia matokeo sahihi wakati unafuga kuku.

Yafuatayo yanapaswa kufanyika kwa mujibu wa  ushauri ninaotoa, kama kuna mtaalamu mwingine anamaoni nakaribisha ili tujenge nyumba IMARA
.
Majukumu ya kila siku
👉Usafi wa vyambo vya maji
👉Ulishaji wa kuku kwa wakati
👉Usafi wa stoo ya chakula
👉Kuchunguza maendeleo ya kuku
👉Kupitia ratiba za chanjo
👉Kusafisha vitagio/viota
👉Kuokota mayai kwa muda sahihi
👉Kuhakikisha dawa za panya zimewekwa kuzunguka banda
👉Kutoa kuku waliokufa bandani na kuwateketeza
👉Kugeuza maranda
👉Kubadilisha maji ya kukanyaga mlangoni

Majukumu ya kila wiki
👉Kupima uzito wa kuku
👉Kufanya hesabu ya matumizi ya wiki kwa kila huduma
👉Kupiga hesabu ya mapato na matumizi
👉Usafi wa madirisha na nyavu bandani
👉Kugeuza maranda Folking.
👉Kujiandaa kwa wiki inayo fuata
👉Kutafuta wateja wapya(kama huna mteja wa kudumu).
👉Kujua idadi sahihi ya kuku( kwa kuangalia walio kufa na waliobaki).

Majukumu ya kila mwezi

👉Mwite mtaalamu aangalie maendelo ya kuku wako
👉Chukua sample ya kuku, au kinyesi kupeleka  kwa wataalamu kujua aendeleo ya kuku(Kama unaweza).
👉Fuatilia ratiba za chanjo hakikisha zinafanyika
👉Hakikisha randa ni kavu na haisababishi magonjwa.

👇👇Majukumu mengine

👉Hakikisha dawa za minyoo zimetolewa kwa kuku
👉Chanjo za kila baada ya miezi mitatu zimefanyika
👉Unajua kiwango cha uzalishaji kwa kuku wako
👉Fuatilia mabadiliko yoyote utakayo yaona bandani
👉Jipe muda wa kufurahia mradi wako( Chinja kuku, kaanga mayai kula na Familia)

By KAHISE MTAALAMU WA KUKU
0769799728 0715894582

Pata uchambuzi wa gharama za chakula cha chotara na Layers mwanzo mpaka kuuza kwa 2000 tu SOFT COPY.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...