Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE


MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE

_Note_
Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha.

No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO

_Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani

_Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin.

Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu.

No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE
_Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa

Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus

_Tiba_:Hakuna tiba ni ugonjwa wa virus.

Chanja kuku wako Siku ya 14 na 28

NO 3: MAREK'S DESEASE/ MAHEPE
_Dalili kuu_:kuparalyse /kukakamaa kwa miguu na mbawa, Hapa mguu mmoja mara nyingi huwa mbele na mwingine nyuma,

 kuvimba kwa kiifadhia chakula (crop), kwa kuku wa mayai huathiriwa wakiwa wadogo ila madhara hutokea wakifikisha miezi 5/wakianza kutaga.
_Tiba_:Hakuna tiba ni ugonjwa wa virus.

Chanja vifaranga siku ya kwanza.

NO 4: NDUI YA KUKU / FOWL POX.
_Dalili kuu_:Vipele sehemu zisizokuwa na manyoya kama vile vilemba vya kichwani (comb na wattle), puani na miguuni.

_Tiba_:Hakuna tiba ni ugonjwa wa virus, kupunguza madhara muoshe kwa maji ya uvugu vugu hadi Vipele viishe au vipake mafuta na mpe antibiotic kama Otc 20%.

Chanja kuku wako Siku ya 30 au wiki ya .4 na 5( chanjo ni Mara moja ). Kwenye bawa


No 5: MAFUA MAKALI/ CORYZA
_Dalili kuu_:Chafya, kusinzia, kuvimba uso/kichwa /macho, ute mzito mweupe jichoni hupelekea jicho kuziba, urenda puani na mdomoni.

_Tiba_: Fluban, au  tylodox au Enrovet dawa hizo pia ni vyema kuchanganya na vitamin.

No 6: FOWL TYPHOID/ HOMA YA MATUMBO
_Dalili Kuu_:Mharo rangi ya nyeupe
_Tiba_: Esb3, Trimazine 30%, Limoxin, enrovet, Ganadexel


NO 7: COCCIDIOSIS/ MHARO DAMU
_Dalili kuu: Kinyesi/mharo rangi ya ugoro mwanzo na unavyoendelea kinakuwa rangi ya damu.
_Tiba_: dawa nzuri ni Amprolium 20%,nyingine ni Esb3, Trimazine 30%, vitacox, na agracox

Kuku wakifikia level ya kutoa damu tumia Anticox.

NO 8: FOWL CHOLERA/ KIPINDUPINDU CHA KUKU
_Dalili kuu_: kinyesi mharo wa kijani.
_Tiba_: Tremazine 30 % au Esb3.

MAGONJWA MATATIZO YANAYOTOKAN NA LISHE DUNI
NO 9_Kuvimba macho, miguu kukosa nguvu na kashindwa kusimama au kutembea, kutaga mayai tepetepe, kula mayai, kudonoana.
_Tiba_: Chakula kiwe na mchanganyiko mzuri wa vitamin, making, na protein, kwa wanaodonoana kata au choma midomo yao.

Imeandaliwa na
Greyson Kahise
Mtaalamu wa kuku
0769799728 0715894582

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...