Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONO YAHUSUYO UFUGAJI


WAZO LANGU SIKU ZA USONI

INASIKISHA!INAHUZUNISHA!!KUONA

Makampuni yanashusha bei za vifaranga,,,vyakula vinapanda bei,,,lakini kuku wanashuka bei bandani na sokoni kila siku,,,,wakati mlaji wa mwisho amekua akiuziwa kuku kwa bei ileilee ya tangu zamani wafugaji tunaumia sana

MAONO NA MTAZAMO NI KUWA NA UMOJA KAMA WAFUGAJI KUKU KILA MKOA

Naamini kila mkoa kuna umoja wa wafugaji wa kuku au kama hakuna umoja wa kila mikoa kupitia groups hizi za kuku nitajitahidi kushawishi kwa kadri nitakavo weza umoja uundwe

Kilaa mkoa wafugaji wa kuku tujuane..tuwe na uongozi...tuwe tunafanya makubaliano hasa ya masoko kutokana na mabadiliko ya bei ya vyakula na vifaranga

Badaa ya muda nitaandaa links ambazo wafugaji wa mkoa husika watakua wakijoin na kuwasambazia wenzao kisha huko watapatikana wa kuzisimamia izo groups hatimae tuwe kitu kimoja kila Mkoa

Hii itasaidia saana huko mbeleni hata kuwa na sauti kwenye soko...kwa kujiwekea msimamo wa uuzaji wa kuku

Tukumbuke wanunuzi wa kuku huja bandani na bei zao wakijua wafugaji nilazima tuuze kwasababu kuku wakibaki bandani tutapata hasara

Ilaa huko mbeleni kama tutafanikiwa kuwa na msemaji wa kilaa mkoa na makubaliano ya kila mkoa itatufanya tuwe huru na msimamo hatimae KUKU WATUPE FAIDA

Nafahamu mwanzo wa kulianzisha hili ni mgumu ilaa mpaka sasa nimeanza kwa sehemu na mwitikio ni mkubwa sana

KARIBU TUUNGANE TUUPINGE HUU UKANDAMIZWAJI WA WAFUGAJI WADOGO

Greyson kahise  0769799728/0653387629

KUKU TAIFA KUBWA TUKIUNGANA TUNAWEZA TUUNGANE

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...