Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONO YAHUSUYO UFUGAJI


WAZO LANGU SIKU ZA USONI

INASIKISHA!INAHUZUNISHA!!KUONA

Makampuni yanashusha bei za vifaranga,,,vyakula vinapanda bei,,,lakini kuku wanashuka bei bandani na sokoni kila siku,,,,wakati mlaji wa mwisho amekua akiuziwa kuku kwa bei ileilee ya tangu zamani wafugaji tunaumia sana

MAONO NA MTAZAMO NI KUWA NA UMOJA KAMA WAFUGAJI KUKU KILA MKOA

Naamini kila mkoa kuna umoja wa wafugaji wa kuku au kama hakuna umoja wa kila mikoa kupitia groups hizi za kuku nitajitahidi kushawishi kwa kadri nitakavo weza umoja uundwe

Kilaa mkoa wafugaji wa kuku tujuane..tuwe na uongozi...tuwe tunafanya makubaliano hasa ya masoko kutokana na mabadiliko ya bei ya vyakula na vifaranga

Badaa ya muda nitaandaa links ambazo wafugaji wa mkoa husika watakua wakijoin na kuwasambazia wenzao kisha huko watapatikana wa kuzisimamia izo groups hatimae tuwe kitu kimoja kila Mkoa

Hii itasaidia saana huko mbeleni hata kuwa na sauti kwenye soko...kwa kujiwekea msimamo wa uuzaji wa kuku

Tukumbuke wanunuzi wa kuku huja bandani na bei zao wakijua wafugaji nilazima tuuze kwasababu kuku wakibaki bandani tutapata hasara

Ilaa huko mbeleni kama tutafanikiwa kuwa na msemaji wa kilaa mkoa na makubaliano ya kila mkoa itatufanya tuwe huru na msimamo hatimae KUKU WATUPE FAIDA

Nafahamu mwanzo wa kulianzisha hili ni mgumu ilaa mpaka sasa nimeanza kwa sehemu na mwitikio ni mkubwa sana

KARIBU TUUNGANE TUUPINGE HUU UKANDAMIZWAJI WA WAFUGAJI WADOGO

Greyson kahise  0769799728/0653387629

KUKU TAIFA KUBWA TUKIUNGANA TUNAWEZA TUUNGANE

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...