Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MWONGOZO WA KUKU WA MAYAI

MWONGOZO WA KUKU WA MAYAI.

👉Kuku wa mayai, hawa ni kuku ambao vinasaba vyao huwawezesha kutaga mayai mengi kwa muda watakao fugwa

Zipo aina nyingi za kuku wa mayai hapa nitataja baadhi

👆Hy-line, Isa brown, Bavon brown, Lohman brown, Rhode Island n.k

Yapo mambo kadhaa ya kuzingatia kwa kuku wa mayai

👏ENEO
👉Idadi ya kuku kwa mita moja mraba ni kuku 7-8 ndio inayo shauriwa sana kitaalamu kwa ukuaji na kuzunguka

👉Vyombo vya chakula na maji

Belly drinker 1 kuku 60-80

Chicken /feeder drinker kubwa Lita 20 kuku 50-60

Chicken  drinker/feeder ndogo lita 10 kuku 20-25

Hii huwezesha kuku kupata maji ya kutosha

👉👈NB : Kuku anatakiwa kunywa maji zaidi ya Mara mbili ya chakula anachokula kwakua zaidi ya 75% ya yai ni maji, ukipunguza maji wanapunguza kutaga
ZINGATIA

👉Kuku wapewe chakula kwa ratiba sahihi iliyo zoeleka usibadilishe ratiba utawastress na wataounguza kutaga

👉Mfano huwa unalisha saa 6 AM na 4 PM hakikisha unawalisha kila Siku muda huo

👏Kuku walishwe kwa mfumo wa gramu ili kuzuia kujaza mafuta au kutumia chakula kingi kuzalisha yai moja, kwa kawaida kuku mmoja wa mayai anatakiwa kukupa mayai 6-7 kwa kilo 1 ya chakula (Hyline)

Mfn: Unakuku 100, wiki ya 20, wanatakiwa kula gram 120 kwa kuku mmoja
👉👈Chukua 120× 100=12000gram
👆12000/1000=12 kg
Kwahiyo kuku hao wiki hilo watakula Kilo 12 za chakula kwa siku.

Kuku wana pitia stage 3

Brooding wakiwa vifaranga mpaka wiki 4,

Growing wiki 5 -17 na Production baada ya kuanza kutaga mayai

Hivi vipindi vinatofautiana kiuangalizi na kipindi cha kutaga hutegemea vipindi hivi( Brooding au malezi ya vifaranga na Growing)

Brooding zingatia
Chakula, Joto, hewa safi, Mwanga, nafasi ya kukaa inashauriwa 40 chicks kwa 1m2( vifaranga 40-60 kwa mita 1 mraba)

Growing
Zingatia chakula, Mwanga , nafasi na Hewa safi kwakua hapa ndo kuku anakua anaandaa mfumo mzima wa mayai

CHAKULA

👉Starter kwa wiki1- 6/8

👉Grower 7/8-17 au watakapo anza kutaga

👉Layers mash baada ya kuokota yai nakuendelea,  hii huanza Mara nyingi wiki ya 18-20 ndipo kuku wengi huanza kutaga.

👏👈Kuku wakianza kutaga nivema ukawapa masaa 16 ya Mwanga kama somo la mwanga linavoelekeza yaani ,mchana masaa 12 mwanga wajua ,kisha jioni unawasha taa na kuizima saa 4 usiku.

Ratiba za chanjo

👉Siku ya 7na 21 Newcastle (ya maji au matone) (LASOTA)

👉Siku ya 14na 28 gumboro( Ya maji)

👉Siku ya 30ndui(Ya bawa)

👉Kila baada ya miezi 3 rudia chanjo ya Newcastle

👉Wape dawa za minyoo kila baada ya miezi mitatu.mfn Piperazine, Levifarm, Fenbemdazole, (Mtafute Daktari wa mifugo)

👆👇USHAURI
👉Uza mayai na uweke akiba kwaajili ya kuingiza kuku wengine , tunashauri uingize kuku kwa kutofautisha rika hii itakusaidia kukuza mradi pia kuwawezesha wateja wako kupata huduma muda wote.

👉Weka kumbukumbu ya gharama zote ulizotumia

👉Chanjo za maji, ziwekwe kwa masaa mawili pekee, kisha badilisha maji na kuweka maji mengine (yanaweza kuwa na vitamin au maji matupu), ila watolee maji masaa 2 kabla ya kuwapa chanjo na uwape chakula kuongeza kiu, (inashauriwa kuchanja Asubuhi au jioni)

👉Fuatilia kwa makini idadi ya vifo ,ili ujue kuku waliobaki kupima uzalishaji( usipokua makini utaibiwa)

👉Epuka kutumia dawa bila kumshirikisha Daktari wa mifugo, dawa nyingine hupunguza au kukata utagaji mayai kwa muda , Zenye salfa kama Esb 3 n.k.

👉Hakikisha randa bandani haziloani, kuepusha magonjwa ya Coccidiosis,  na ya kuumia miguu kwa kuunguzwa na Ammonia bandani.

👉Fanya tathmini ya mradi Mara kwa Mara, angalau kila mwezi

👉Jitahidi sana kutafuta taarifa za masoko mkoani kwako na mikoa mingine , kupanda, kushuka kwa soko ili uweze kuuza kwa bei zilizopo (Usiwe nyuma)

👉Wahudumu wa kuku, wapate huduma zote za msingi kama wanao , usiweke GEP baina yao na familia , watapenda kazi na uzalishaji utakua mzuri na hawataiba ( Boresha maslahi)

👉Zingatia sana sheria za Viumbe hai salama, BIOSECURITY kupunguza case za magonjwa

👉👆 Kwa wanaofuga kwa cages.
👉Huu ni mfumo mzuri na rahisi kwa kuku
👆Mayai masafi
👆Hayapasuki
👆Wafanyakazi wachache
👆Magonjwa hupungua
👆Chakula hakimwagiki sana

👉👆Inashauriwa kuku wawekwe kwenye cages wakifikisha umri wa wiki 12-14, kuzoea mazingira ili wasipate stress.

👆👉👈 Madaktari, wataalamu na wafugaji wazoefu mwaweza ongeza ushauri pia tufikie malengo

👉👆Imeandaliwa na
GREYSON KAHISE
MTAALAMU WA KUKU
0769799728 0715894582

NUNUA KITABU CHA FUGA KUKU KITAALAMU KIMEELEZEA VEMA ZAIDI.*  10000 mikoa yote TZ

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...