Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UTAMBUZI WA KUKU WANAOTAGA NA WASIOTAGA

NIWATAMBUAJE KUKU WASIOTAGA

👈Kwanza kabisa , ni kusudi la kila mfugaji anaejihusisha na ufugaji wa kuku wa mayai, au kienyeji au chotara kupata mayai ndani ya muda kutokana na aina ya kuku anao wafuga.

👈Kwakua inafahamika hivo, wafugaji wengi tumekua tukitarajia kuku wetu kuanza kutaga ndani ya muda tulio kusudia

Kwa kawaida muda wa kutaga kuku kwa uzoefu wangu umetofautiana na maranyingi imekua kama ifuatavyo

👉Kuku pure wa mayai mfn. Isa Brown, Lohmann Brown, Hy-line nk wamekua wakianza kutaga wiki ya 17-18-19 na (20  kwa kuchelewa)

👉Kuku chotara kama ,Kuloirer, Sasso, Tanbro kuanzia wiki ya 18-21 wanakua wameanza kutaga.

👉Kuku wa pure kienyeji wamekua wakianza kutaga wiki 24 yaani miezi 6.

👆👆Kuwahi au kuchelewa kuanza kutaga kunategemea hasa vitu vifuatavyo
👉Ubora wa chakula, Wakipewa chakula sahihi tangu udogoni watataga kwa wakati, ukikosea lazima wasumbue kutaga

👉Mwanga, Masaa sahihi ya mwanga wakati wa ukuaji, na pindi wanapo anza kutaga, kiusahihi kuku apate masaa 16 ya mwanga baada ya kuanza kutaga.(washa taa sa 12 jioni na wazimie taa saa 4 usiku).

👉Maji, yawepo maji muda wote kwani zaidi ya 75% ya yai inachukuliwa na maji.

👉Magonjwa, wachanje kuku wako ipasavyo na upunguze uwezekano wa magonjwa kuwapata kuku muda wote, hivo utatumia dawa Mara chache hawata sumbua kuanza kutaga.

👈👉Hakika kama utazingatia hayo uwezekano wa kuku kuanza kutaga ndani ya wakati ni mkubwa sana.

👆👆Maranyingi kuku waliokuzwa vizuri kwa uwiano huchukua kati ya mwezi mmoja tangu kuanza kutaga mpaka kufika Peak/ kiwango cha juu cha utagaji , ila kutokana na changamoto za ufugaji wa kwetu wengi wamekua wakikaa miezi 2 ndipo wafike kiwango cha juu cha utagaji.

☑️Binafsi Kuloirer wangu walianza kutaga wiki ya 19, na walikaa mwezi mmoja na wiki moja kufika Peak ya utagaji.

UNATAMBUAJE KUKU WANAOTAGA

👉Njia ya kupitisha yai/nyonya hufunguka na huruhusu vidole zaidi ya viwili ukivilaza kulala, ( ambae hatagi njia inakua haijafunguka )

👉Anaetaga Vent/anapotolea yai huwa na unyevu unyevu muda mwingi (asietaga panakua pakavu muda mwingi)

👉Kuku anaetaga Vent/ sehemu inapotokea yai huwa na rangi kama nyekundu, ila asietaga huwa peupe (Unaweza baini ukiwa unafanya uchunguzi practically)

👉Kuku anaetaga Mlango wa kutolea yai hutanuka , asietaga hautanuki sana.

👉Kuku anaetaga Kilemba huwa chekundu cha kuiva kuliko yule asietaga

👉Kuku anaetaga huwa mzito na mtulivu, asietaga huwa mwepesi na machachali sana (machepele).

👏Nimejitahidi kusema ninavo vifahamu kwa uzoefu wangu kama kuna mtaalamu au mfugaji mwingine anauzoefu zaidi anaweza kutuwezesha kwa elimu.

Imeandaliwa na
GREYSON KAHISE
MTAALAMU WA KUKU
0715894582 0769799728

KARIBU TUKUHUDUMIE.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAGONJWA MAKUU YA KUKU DALILI NA TIBA ZAKE

MAGONJWA MAKUU YA KUKU, DALILI, NA TIBA ZAKE _Note_ Katika dalili za magonjwa nitakayowaandikieni kitaalamu huwa Kuna dalili kuu na zisizo kuu, dalili kuu maana yake ni dalili ambayo ukiiona inakupa ukweli halisi kuwa huu ni ugonjwa fulani na huwa hazifanani kamwe, zisizo kuu ni zile zinazofanana kwa mfano kushusha mbawa, kukosa hamu ya kula, kuzubaa n.k  dalili kama hizi kila kuku mgonjwa huzionyesha. No 1:NEWCASTLE /KIDERI/ MDONDO _Dalili kuu_: Kupindia shingo juu au chini, mwendo wa kuzungukazunguka, kutembea mwendo wa kurudi nyuma huku kichwa kikiwa kimepindia chini au juu. Dalili isiyo kuu ni mharo rangi ya kijani _Tiba_: Hakuna tiba huu ni ugonjwa wa virus kinachotibika ni hizo dalili tu ila ugonjwa hubaki kwenye damu hivyo tumia Trimazine 30%+vitamin. Chanja kuku wako, siku ya 7, 21 na rudia baada ya miezi mitatu. No 2: GUMBORO/ INFECTIOUS BURSAL DISEASE _Dalili kuu_:Mharo rangi nyeupe hukauka kama chokaa Postmortum; Huonesha uvimbe wa bursal of fabricus _Tiba_:Hakuna tiba n...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MAKALA JUU YA MAYAI/YA KUKU NA UTOTOLESHAJI

Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21 kabla ya vifaranga kutotlewa  ilhali bata  hutotoa baada ya siku 28 Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)      Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)      Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3)      Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga vyenye afya mbaya au vilivyokufa. 4)      Hifadh...