Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUDONOANA NA KULA MAYAI

MAKALA KUHUSU KUKU KULA MAYAI, KUDONOANA NA KUNYONYOKA MANYOYA

Tatizo la kuku kuwa na tabia zisizo faa/cannibalism limekua shida kubwa kwa wafugaji wengi wa kuku aina zote, ilaa limekua likijitokeza sana hasa kwa kuku wa mayai

Tatizo hili pia limekua likijitokeza kwa kuku wa rika tofauti tofauti..ilaa linazidi pale kuku wanapo anza kutaga mayai

 Chanzo cha tatizo

Kuku kuwa wengi kwenye banda dogo kuzidi uwezo wa banda kuhifadhi kuku

Kukosekana kwa vifaa vya kutosha vya chakula na maji pia kuku kukosa chakula cha kutosha

Upungufu wa protini, na madini kama calcium kwenye chakula cha kuku

Kuwa na idadi kubwa ya majogoo bandani kuzidi idadi inayotakiwa

Kuku kuchoka au kuzeeka pale muda wake utakapo kua umefika mwishoni

 SULUHISHO

Kwa kuku anaekula mayai, mwongezee kiwango cha chakula chenye protein kwenye chakula kama soya meal na dagaa,,,pia mwongezee vitamins kuku wako atapunguza kula mayai pia waongezee kiwango cha mifupa au chokaa kwenye chakula chao,,kama utatumia magamba ya konokono hakikisha usalama wake maana wakati mwingine hupelekea Typhoid

Kwa kuku wanao donoana, weka kiwango sahihi cha vifaa vya maji na chakula, weka idadi sahihi ya kuku bandani wapate nafasi, wawekee majani muda fulani ili chakula kikiisha wawe busy kula wasipate muda wa kudonoana

Kwa kudonoana na kula mayai..endapo utatumia mbinu zote hapo juu na isisaidie njia ya mwisho kabisa ni kuwakata kuku midomo kwa kutumia kifaa maalumu cha kukatia midomo de-beacker...au kuchoma mdomo kwa njia za kienyeji...baada ya kuwakata midomo wape chakula kingi na vitamins kwa wingi

Kwa kuku wanao nyonyoka manyoya, waweke jogoo kwa uwiano na tetea,,jogooo mmoja kwa tetea 8-10, wape chakula chenye mchanganyiko wa madini ya calcium, zuia wadudu kama utitiri viroboto au kupe kwa kupulizia dawa ya Akheri powder au Paranex piaa usafi bandani uwe wakuridhisha.

Kikubwa cha kufahamu hapa ukifuatilia kwa makini hizi changamoto huwapata zaidi kuku ambao wafugaji hujichanganyia chakula chao, hivo ni vema ukachanganya chakula kutokana na uhitaji wa kuku na umri wa kuku na utumie formula sahihi ya mchanganyiko wa chakula

 Imeandaliwa na Greyson Kahise mtaalamu wa kuku 0769799728...Karibu nikuhudumie kwa uzalishaji bora wa kuku na mayai

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...