Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

HATUA ZA KUFUATA KUANZISHA MRADI WA KUKU

HATUA ZA KUFUATA ILI KUANZISHA MRADI WA KUKU. 👆Kutokana na wengi sana kunitafuta kuomba ushauri, hasa wafugaji wageni au wapya wanao anza kwamba waanzaje mradi wa kuku 👇Zifuatazo ni hatua sahihi za kufuata ili kuwa na mradi endelevu wa kuku 👉Moja Jenga banda la kufugia kuku wako, Kabla ya kufanya kitu chochote hakikisha umejenga banda, au umepata nyumba ambapo mradi wako wa kuku utajengwa, ukubwa wa banda utategemea 👈Uwezo kifedha 👈Malengo ya uwekezaji 👈Urahisi wa upatikanaji bidhaa Ukisha jenga banda au kujihakikishia kwamba kuku wako watakaa wapi kisha FUATA hatua hizi 👆Mbili. Tafuta vifaranga, au mayai na utotoleshe , au kununua kuku wa rika yoyote utakayo pendelea kulingana na Uwezo wako kifedha pia kuzingatia banda ulilo lijenga 👈Kiusahihi zaidi ni vema kununua Vifaranga, au mayai ya kutotolesha kutoka shamba unaloliamini kuliko kununua kuku wakubwa👏 👆Tatu Hakikisha unao uwezo, au umefanya makadirio ya kuhudumia mradi hasa kwa miezi mitano ya kwanza kabla ya kuku kuanza ...

JINSI YA KUTENGENEZA SEHEMU YA KULELEA VIFARANGA/ BROODER

MAANDALIZI YA SEHEMU YA KULELE VIFARANGA/ BROODING AREA 👆Brooder ( kinengunengu), hii ni sehemu ya muhimu sana , na yakuzingatia sana wakati wa malezi ya vifaranga  SIFA ZA BROODER 👉Joto lakutosha 👉Randa/matandazo 👉Maji 👉Chakula 👉Hewa ya kutosha 👉Mwanga 👉Nafasi ya sahihi ya kutosha 👉👇nini sasa ufanye kuandaa brooder/ sehemu ya kulelea vifaranga. 👉Kwanza angalia idadi ya vifaranga wako, 👈Brooder inaweza kuwa ya duara, kama utalea vifaranga wachache 👈Kama utalea vifaranga wengi unaweza kutengeneza brooder ya pembe nne kwa kuzingatia vipimo. MATENGENEZO YA BROODER YA DUARA 👉Tafuta siling board, ikate kwa urefu vipande vitatu (standard 30-40 cm) kimo, au wengine hukata Mara mbili *(katikati)* 👉Unganisha vipande ulivyo vikata kutengeneza duara lako, Mimi huunganisha kwa kuchana kibao kwa msumeno kitakacho shikilia siling board upande wa juu kwenye maungio. 👉Kitaalamu mita moja mraba hutosha vifaranga 40, ila eneo utakua unalitanua kwa kadri vifaranga watakavo kua wanaong...

NINI UFANYE KWA KUKU WA MAYAI WAKATI WA BARIDI

MREJESHO WA UTAFITI NA KUJUMLISHA KNOWLEDGE NILIYONAYO 👆Nimepokea report nyingi sana za kuku kushusha utagaji kwa kiwango kikubwa msimu huu (wanaotumia vyakula vya viwandani ,pia wanaojitengenezea ) nafikiri ni baridi imesabanisha 🙏Je huwa unapambanaje na hali hii kuepuka hasara msimu huu, 👆Kwanza nishukuru kwa wote mliotoa michango yenu mbalimbali kuhusu swali langu hapo juu. 🙏Kwanza kabisa nini hutokea, Kipindi cha baridi, mwili wa mnyama mwenye damu moto, huhitaji Joto kusawaza kiwango cha joto la mwili 👈Hivyo hivyo kwa kuku,, huhitaji kiwango cha joto laziada kipindi hiki kukidhi joto la mwili (40°c) 👆👆 IKUMBUKWE 👉Kuku anaetaga anahitaji Enegy/ wanga kwaajili ya vitu viwili 🐣Production/Uzalishaji 🐣Maintanance/Kulinda mwili 👉Hivyo basi chakula anacho kula kuku, kinagawanyika sehemu hizo 2, 👆Wakati wa baridi kuku anahitaji kiwango kikubwa cha chakula kujilinda au kuzalisha joto la mwili, na kinachobaki ndicho hutumika kutengeneza yai 🐣Ikumbukwe kiwango cha chakula ulicho...

MWONGOZO WA KUKU WA MAYAI

MWONGOZO WA KUKU WA MAYAI. 👉Kuku wa mayai, hawa ni kuku ambao vinasaba vyao huwawezesha kutaga mayai mengi kwa muda watakao fugwa Zipo aina nyingi za kuku wa mayai hapa nitataja baadhi 👆Hy-line, Isa brown, Bavon brown, Lohman brown, Rhode Island n.k Yapo mambo kadhaa ya kuzingatia kwa kuku wa mayai 👏ENEO 👉Idadi ya kuku kwa mita moja mraba ni kuku 7-8 ndio inayo shauriwa sana kitaalamu kwa ukuaji na kuzunguka 👉Vyombo vya chakula na maji Belly drinker 1 kuku 60-80 Chicken /feeder drinker kubwa Lita 20 kuku 50-60 Chicken  drinker/feeder ndogo lita 10 kuku 20-25 Hii huwezesha kuku kupata maji ya kutosha 👉👈NB : Kuku anatakiwa kunywa maji zaidi ya Mara mbili ya chakula anachokula kwakua zaidi ya 75% ya yai ni maji, ukipunguza maji wanapunguza kutaga ZINGATIA 👉Kuku wapewe chakula kwa ratiba sahihi iliyo zoeleka usibadilishe ratiba utawastress na wataounguza kutaga 👉Mfano huwa unalisha saa 6 AM na 4 PM hakikisha unawalisha kila Siku muda huo 👏Kuku walishwe kwa mfumo wa gramu ili ...

UTOTOLESHAJI WA MAYAI NA KUHIFADHI

👉👈Mayai ya kuku huanguliwa kwa siku 21, ila zoezi la mayai kuanguliwa huanza mapema siku ya 18-21, na mayai yakizidi siku 21 Mara nyingi huwa yameharibika. 👉Uatamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga: Mayai kwa ajili ya kuatamiwa ni lazima yawe mapya; 1)Umri wa mayai baada ya kutagwa usiwe zaidi ya siku kumi (10) na yawe yamehifadhiwa katika sehemu yenye ubaridi usiozidi nyuzi joto 20ºC .Iwapo hali ya joto iko juu kuliko 20ºC basi mayai ya kutotoa vifaranga yasihifadhiwe kwa zaidi ya siku tano (5). 2)Ili kupata matokeo mazuri, mayai ya kuatamiwa (mayai yaliyochaguliwa) yanatakiwa yawe na umbo la kawaida na ukubwa wa wastani kwa aina ya kuku wanaohusika. 3) Ganda la mayai ya kuangua lisiwe na mikwaruzo au nyufa  kwani likiwa na nyufa yai hupoteza unyevunyevu ambao ukipungua kiiini cha yai kinaweza kufa au linaweza kuingiza vimelea kama fangasi na bakteria ambavyo husababisha kutotolewa kwa vifaranga wenye afya mbaya au walio kufa 4)Hifadhi mayai ya kuangua kwenye makasha makavu...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...

KUDONOANA NA KULA MAYAI

MAKALA KUHUSU KUKU KULA MAYAI, KUDONOANA NA KUNYONYOKA MANYOYA Tatizo la kuku kuwa na tabia zisizo faa/cannibalism limekua shida kubwa kwa wafugaji wengi wa kuku aina zote, ilaa limekua likijitokeza sana hasa kwa kuku wa mayai Tatizo hili pia limekua likijitokeza kwa kuku wa rika tofauti tofauti..ilaa linazidi pale kuku wanapo anza kutaga mayai  Chanzo cha tatizo Kuku kuwa wengi kwenye banda dogo kuzidi uwezo wa banda kuhifadhi kuku Kukosekana kwa vifaa vya kutosha vya chakula na maji pia kuku kukosa chakula cha kutosha Upungufu wa protini, na madini kama calcium kwenye chakula cha kuku Kuwa na idadi kubwa ya majogoo bandani kuzidi idadi inayotakiwa Kuku kuchoka au kuzeeka pale muda wake utakapo kua umefika mwishoni  SULUHISHO Kwa kuku anaekula mayai, mwongezee kiwango cha chakula chenye protein kwenye chakula kama soya meal na dagaa,,,pia mwongezee vitamins kuku wako atapunguza kula mayai pia waongezee kiwango cha mifupa au chokaa kwenye chakula chao,,kama utatumia magamba ya...