Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIFA ZA MAYAI YANAYOHITAJIKA/YANAYOFAA KATIKA KIATAMISHI

Wafugaji wengi wamekuwa wakipata hasara kutokana na utotoleshaji mbovu wa mayai kwani mengi huharibika bure. Hayo hutokana na kutozingatia maelekezo ya sifa za mayai bora yanayofaa kuatamiwa na kiatamishi.
Kabla ya kuweka  mayai ndani ya kiatamishi hakikisha mambo yafuatayo yamezingatiwa kikamilifu;
Yai lisizidi siku 7 mpaka 10 tangu litagwe. Hii iina maana kwamba mayai yanayotakiwa kuwekwa kwenye droo ya kiatamishi lazima yawe ni yale ambayo hayajazidi siku 7 au 10 tangu yatagwe na kuku. Hivyo hakikisha suala hili wakati wa ukusanyaji wa mayai yaliyotagwa. Hivyo kama umekusanya mayai muda wa siku 10 mfululizo basi hutakiwi kuongeza tena yai jingine kwakuwa ile siku ya kumi (10) kumbuka tayari kuna mayai ya mwanzo kukusanywa yatakuwa tayari yameshakaa siku 10. Kwahiyo kama utaendelea kukusanya siku zaidi ya 11 basi yai la mwanzo kukusanywa lazima litolewe!
Mayai yahifadhiwe kwenye trei yakitoka kuokotwa bandani.
Zingatia uwiano mzuri wa majogoo kwa matetea (1:8-10)
Mayai ya mtago wa kwanza sio mazuri kwa kutotolesha. Hii ina maana kwamba kama kuku ameanza kutaga leo basi usichukue yai la leo bali anza kuokota yai la siku inayofuata, yaani yai la kwanza sio sahihi kwakuwa huenda likawa halijarutubishwa vizuri.
Mayai ya kuku mzee sio mazuri kwa kutotolesha
Kuku watagaji wanapaswa kupewa chakula bora na cha kutosha
Mayai yahifadhiwe sehemu isio na joto kali
Mayai machafu au yenye madoa ya damu hayafai kwa kutotolesha
Mayai yenye kreki (nyufa) hayafai kwa kutotolesha
Mayai yenye umbo kubwa sana au madogo sana hayafai kwa kutotolesha (yanatakiwa yawe na ukubwa wa wastani).
Mayai yenye viini viwili hayafai kwa kutotolesha
Yai lisihifadhiwe kwenye frigi (hifadhi sehemu yenye hewa ya kutosha na isio na joto kali.)
Mayai yahifadhiwe kwenye matrey.
Wakati unahifadhi mayai katika trei hakikisha sehemu ya yai iliyochongoka inaangalia chini
Tengeneza viota vya kutagia ili kuepusha mayai yasichafuke kuku anapotaga!wala yasiguse maji au kupasukiana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

MATUMIZI YA DAWA KWA KUKU ZINGATIA

MAKALA KUHUSU DAWA KWA KUKU. Leo ni vema kidogo tuelezane kuhusu matumizi ya dawa kwa very good but kuku...hasa Hb kuhusu namna sahihi ya matumizi ya dawa na jinsi ya kuzitumia Kitu cha kwanza ieleweke kwamba dawa sio kinga ila ni tiba ya ugonjwa ambao unakua umeshatokea kwa hiyo ni muhimu kuwapa kuku chanjo za magonjwa Chanjo pia kama haitahifadhiwa katika mazingira sahihi au kutumiwa kwa namna sahihi ubora wake hupungua hivyo ufanisi wake kukinga ugonjwa hupungua vilevile Vitu sahihi kuvijua kabla hujatumiwa dawa yeyote 1.Hakikisha umefahamu ugonjwa upi unaoutibu 2.hakiksha unajua ugonjwa upo katika stage ipi... 3.hakikisha umefanya uchunguzi  juu ya magonjwa mengine yanaohusiana na ugonjwa husika 4. Ni muhimu zaidi kufahamu umri WA kuku wako na kuchagua dawa sahihi kulingana na umri... 5.hakikisha unafahamu level ya uzalishaji na muda kabla ya kuchagua utumie dawa ipi... Mara nyingi kuku akiumwa ugonjwa mmoja huongeza uwezekano WA kuumwa magonjwa mengine Ni muhimu kufanya uchung...

UFUGAJI WA BROILERS/ KUKU WA NYAMA

MWONGOZO WA UFUGAJI WA KUKU WA NYAMA/BROILERS Biashara ya kuku imejikita katika uwanja mpana sana kwa kutegemea aina za kuku, kwa maeneo mengi ya mjini Kuku wa nyama wamekua wakiuzika sana Japo kwa bei isiyo rafiki kwa mfugaji 👉Kwa maeneo mengi wafugaji wamekua wakifuga wakitarajia kuuza kuku kuanzia siku ya 28-30, au kama watachelewa sana basi wasizidi siku 35, japo wapo wengine ambao huuza mapema zaidi ya hapo au kwa kuchelewa kutokana na sababu tofauti tofauti. 👆Mambo ya kuzingatia ili broilers waweze kukua ipasavyo. 👉 Chakula 👆Kwa ukuaji wa haraka wa broiler anatakiwa kupewa chakula muda mwingi wa Siku, kutoka kwa wafugaji wazoefu wa broiler wametoa shuhuda kwamba broiler wawashiwe taa masaa 24 na wapewe maji na chakula. 👏Kwa makadirio ya kuku 100, broilers wamekua wakitumia mifuko ya chakula kama ifuatavyo 👉Broiler starter crumble siku 1-13 mfuko mmoja 👉Broiler Grower Pellets siku 14-22 mifuko miwili 👉Broiler finisher Pellets siku 23-kuuza mifuko miwili NB: Zipo shuhuda kw...