Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

UTAMBUZI WA KUKU WANAOTAGA NA WASIOTAGA

NIWATAMBUAJE KUKU WASIOTAGA 👈Kwanza kabisa , ni kusudi la kila mfugaji anaejihusisha na ufugaji wa kuku wa mayai, au kienyeji au chotara kupata mayai ndani ya muda kutokana na aina ya kuku anao wafuga. 👈Kwakua inafahamika hivo, wafugaji wengi tumekua tukitarajia kuku wetu kuanza kutaga ndani ya muda tulio kusudia Kwa kawaida muda wa kutaga kuku kwa uzoefu wangu umetofautiana na maranyingi imekua kama ifuatavyo 👉Kuku pure wa mayai mfn. Isa Brown, Lohmann Brown, Hy-line nk wamekua wakianza kutaga wiki ya 17-18-19 na (20  kwa kuchelewa) 👉Kuku chotara kama ,Kuloirer, Sasso, Tanbro kuanzia wiki ya 18-21 wanakua wameanza kutaga. 👉Kuku wa pure kienyeji wamekua wakianza kutaga wiki 24 yaani miezi 6. 👆👆Kuwahi au kuchelewa kuanza kutaga kunategemea hasa vitu vifuatavyo 👉Ubora wa chakula, Wakipewa chakula sahihi tangu udogoni watataga kwa wakati, ukikosea lazima wasumbue kutaga 👉Mwanga, Masaa sahihi ya mwanga wakati wa ukuaji, na pindi wanapo anza kutaga, kiusahihi kuku apate masaa 1...

USUGU WA DAWA KWA KUKU

HELOW WAFUGAJI TWENDE SAMBAMBA HAPA Kunakitu kinaitwa usugu wa madawa kwa mifugo na binadamu kwa kingereza DRUG RESISTANCE Kwa mujibu wa tafiti kadha wa kadha hili tatizo limekua likiongezeka siku kwa siku na inasemekena bidhaa zitokanazo na kuku zimechangia kwa sehemu kubwa katika swala hili LINATOKEAJE Kila dawa anayopewa mnyama huwa ina muda wa kukaa na kupotea kwenye nyama au mayai/ withdrawal period Kila dawa unayoitumia imeandikwa utumie nyama au mayai baada ya muda gani nivema kuzingatia saana kwani madhara yake hayapo kwa kuku tu bali huhamia hadi kwa binadamu Tuelewe kuna baadhi ya dawa kwa mfano zinzoua bakteria zikitumika zinabaki mwilini kwa muda tofauti..kama utatumia bidhaa yanye kiwango kikubwa chenye dawa...madhara yake nikwamba vimelea wa magonjwa husika huwa sugu na kutosikia dawa na hii inakuja kupelekea hatakama utatumia dawa ya aina hiyo haitafanya kazi tena utalazimika kutumia dawa nyingine kwahiyo garama inapanda maradufu Piaa kutumia dawa isiyo sahihi kwa ugonjw...

NUKUU ZA KUZINGATIA WAKATI WA KUTENGENEZA CHAKULA

WACHA NIKUFUMBUE MACHO KIDOGO Hivi unajua ni kwanini watu husema chakula cha kuchanganya/kutengeneza mwenyewe kina magonjwa mengi??. 👉Sababu ni moja tu..mfugaji anakua hajafanya maandalizi mapema kukabili upungufu wa chakula hali inayo pelekea kununua malighafi ghafla bila kuchunguza ubora kwa msukumo wa kuku kukosa chakula CHAKUFANYA ILI CHAKULA CHA KUTENGENEZA KISIKUSUMBUE 👏Unatakiwa kuandaa malighafi zako za kuchanganyia mapema bila kuwa na msukumo kutoka kwa kuku..hii itakuwezesha kuchagua malighafi bora na safi kwa kuku wako 👉Uchaguzi wa pumba ufanyike kwa umakini kwa kuzingatia ukavu wa pumba utakayo itumia isiwe na uvundo kwani kuku hupata magonjwa tofauti tofauti 👉Kama utatumia dagaa..hapa ndipo pakua makini usitumie dagaa wenye uvundo piaa tumia dagaa kwa kiwango sahihi..ukikosea hapa kuku wako wataumwa typhoid muda wote 👉Damu kitaalamu inakiwango kikubwa cha protini....lakini ni si salama sana kwa afya ya kuku kwani maandalizi ya damu hasa nchini sio yanayozingatia usafi...

SIFA ZA NYUMBA YA KUKU.

NYUMBA YA KUISHI KUKU/POULTRY HOUSE Kwanini nimeamua kuita nyumba ya kuishi kuku/poultry house. Sababu ni kwamba sehemu kuku anapoishi panatakiwa kuwa na vigezo vyote stahiki, ili kumpa kuku uhusu wa kuishi, na kumkinga dhidi ya magonjwa na wanyama wengine hatari kwake.  Nyumba ya kuku inatakiwa kuwa na vitu viuatavyo 👉 Paa Liezekwe kwa Bati, nyasi, Trubai au kitu chochote kitakacho zuia maji, miale ya jua , ndege kuingia bandani. 👉 Sakafu Iwe imara na rahisi kusafishika, kwa kutegemea uwezo na aina ya banda Sakafu pendekezwa ni ile yenye Rough Cement ili kuruhusu unyevu kufyonzwa, pia unaweza jenga na kupaka (udongo wa kichuguu) maeneo ya vijijini.  👉Madirisha Yajengwe mapana, kwa wavu kuruhusu upepo kuingia na kutoka, hii hisaidia kuondolewa kwa hewa zisizotakiwa kama Ammonia Gas. 👆Madirisha yanatakiwa kuwepo pande kuu 2 za banda (Pande ndefu/ ubavuni). 👆Nyavu zinaweza kushikiliwa kwa mbao, miti migumu au kukajengwa tofali course nyembamba kulingana na ramani ya Banda l...

USHAURI

PITIA HII STORI PENGINE ITAKUFAA. 👆Mimi na rafiki yangu mzuri na wa karibu sana, ambae tulianza wote Shule ya msingi, tulicheza mpira wote na siri zetu nyingi za utotoni (kwa kifupi alikua rafiki yangu mkubwa sana ) 👆Tuliondoka nyumbani kwenda kuvua samaki mtoni, tulivogika mtoni, tulianza zoezi la kuvua samaki kwa ndoana, Mungu si Athumani, rafiki yangu alibahatika kupata samaki 11, wakubwa na wazuri , Ila Mimi binafsi nilihangaika sana nakupata samaki mmoja mdogo sana , Kiukweli nililia sana siku ile. 👆Kilicho niumiza ilikua KIU ya kutaka kupata samaki kama mwenzangu, Pia ilikua hasira ya wivu juu ya Samaki wa rafiki yangu 🙏Ila rafiki yangu alinitia moyo akasema hivi, USIJALI ipo siku nawewe utafanikiwa , Ninacho kusaidia nakupatia SAMAKI WATANO, ukienda nyumbani utawambia umevua samaki Sita na Mimi nitasema hivo pia. 👇Lengo la rafiki yangu hapa ilikua kunijengea furaha ya moyo japo kwa uongo, ila pia alikusudia pia kunijengea moyo wa kuto kata tamaa 👇👉 Nini nataka Kusema 👆Ku...

UMUHIMU WA VITAMINI KWA KUKU

JE UNAJUA UMUHIMU WA VITAMIN KWA KUKU UKOSEFU wa VITAMIN kwa Kuku au Upungufu wa VITAMIN hujionyesha kwa namna tofauti katika miili ya kuku, na kila dalili huashiri upungufu wa vitamin. 📌 UMUHIMU WA VITAMINI. - Husaidia katika ukuaji wa kuku. - Humfanya kuku muda wote kuwa amechangamka. - Husaidia kuku kuwa mwenye afya. - Huwezesha kuku kuwa mtagaji Mzuri. 📌 UKOSEFU WA VITAMIN 'A' KWA KUKU Ukosefu wa vtamin 'A' hujitokeza baada ya kuku kukosa vyakula vyenye vitamin 'A' kwa muda mrefu Kuku wadogo huathirika zaidi kwa kwa ukosefu wa vitamun 'A' pia hata kuku wakubwa. 📌 DALILI ZA UKOSEFU WA VITAMIN 'A' KWA KUKU -Macho huvimba na kutoa uchafu mzito kama sabuni ya mche iliyolowana maji -Hudhoofika na hatimaye kufa 📌 TIBA NA KINGA -Kinga ugonjwa huu kwa kuwapa kuku majani mabichi au mchicha au chainizi wakati wa kiangazi au kwa kuku wanaofungiwa ndani na hawawezi kula majani -Wape kuku vitamini za kuku za duka I wakati majani hayapatikani -Kwa kuku...

HATUA ZA KUFUATA KUANZISHA MRADI WA KUKU

HATUA ZA KUFUATA ILI KUANZISHA MRADI WA KUKU. 👆Kutokana na wengi sana kunitafuta kuomba ushauri, hasa wafugaji wageni au wapya wanao anza kwamba waanzaje mradi wa kuku 👇Zifuatazo ni hatua sahihi za kufuata ili kuwa na mradi endelevu wa kuku 👉Moja Jenga banda la kufugia kuku wako, Kabla ya kufanya kitu chochote hakikisha umejenga banda, au umepata nyumba ambapo mradi wako wa kuku utajengwa, ukubwa wa banda utategemea 👈Uwezo kifedha 👈Malengo ya uwekezaji 👈Urahisi wa upatikanaji bidhaa Ukisha jenga banda au kujihakikishia kwamba kuku wako watakaa wapi kisha FUATA hatua hizi 👆Mbili. Tafuta vifaranga, au mayai na utotoleshe , au kununua kuku wa rika yoyote utakayo pendelea kulingana na Uwezo wako kifedha pia kuzingatia banda ulilo lijenga 👈Kiusahihi zaidi ni vema kununua Vifaranga, au mayai ya kutotolesha kutoka shamba unaloliamini kuliko kununua kuku wakubwa👏 👆Tatu Hakikisha unao uwezo, au umefanya makadirio ya kuhudumia mradi hasa kwa miezi mitano ya kwanza kabla ya kuku kuanza ...