Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

VENT PROLAPSE

VENT PROLAPSE Baada ya kuwa nimekua nikipewa case mbali mbali za kuku wa umri tofauti tofauti kuwa na matatizo ya sehemu ya kutolea kinyesi/yai kwa kuku (Vent) kutoka nje nimeona vema leo tuelekezane kidogo. Vent prolapse inaweza kuwatokea kuku wa umri wowote, japo kwa asilimia kubwa tatizo hili limekua likiwatokea sana  kuku wakubwa ( wanaotaga) Vent Prolapse kwa Broilers au kuku wa umri mdogo Kuku hawa huanza kuonesha dalili za sehemu ya kutolea kinyesi kutokeza kwa nje na kushindwa kurudi ndani katika umri tofauti tofauti. Sababu kuu imekua ni upungufu wa madini ya calcium ambayo hufanya misuli ya ndani kushindwa kukaza na kulegea inavo takiwa hivo kuruhusu sehemu ya vent kutokeza nje. Suluhu Kuku watakao onesha hali hii, wapewe chanzo cha madini ya calcium hasa katika hali ya kimiminika Mfn Solucal au DCP iliyo changanywa na maji. Na pia hakikisha kuku aliepata hali hii anatengwa mbali na wenzake ili asidonolewe, pia apewe vitamin na Ant biotic eg OTC . PROLAPSE KWA KUKU WAKUBW...

MUHTASARI WA UFUGAJI KUKU KWA MUJIBU WA KAHISE GREYSON.

1: Maandalizi ya banda la kuku, Fagia, deki kwa maji, pulizia dawa/disinfection (Th4, V rid,Farm guard nk). Acha banda likae zaidi ya siku 7 baada ya kutoa kuku wakubwa kabla ya kuingiza kuku wengine. Andaa vifaa vyote muhimu kwa ajili ya kupokea kuku wapya vikae bandani angalau siku 3 kabla ya kupokea vifaranga. Andaa sehemu ya kulelea vifaranga, weka vyanzo vya joto tayari kabla vifaranga hawajafika(Usikurupuke kuweka wakati vifaranga wameshafika). 2: Maandalizi ya chakula na maji Hakikisha maji, chakula kwaajili ya kuku wako yapo bandani au sehemu ya karibu muda wote ili kurahisisha ulishaji wa kuku. Chimba kisima au weka tank la kuhifadhia maji na uwe na stoo ya kuhifadhia chakula ( isiruhusu panya kuingia ) Hakikisha kuku wamepewa chakula muda sahihi na kwa kiwango sahihi kulingana na umri na aina ya kuku wako. 3: Idadi ya kuku bandani. Ili kupelekea ukuaji murua wa kuku, zingatia nafasi sahihi (idadi sahihi ya kuku kwa mita 1 mraba) Mfano( Pure layers 7-8 kwa 1m², Chotara na kien...

MWONGOZO WA MANUNUZI YA KUKU NA UCHANGANYAJI WAO KWENYE KUKU WENYEJI.

1: Fuatilia kujua historia ya hao kuku hasa katika vipengele vifuatavyo -Chanjo -Magonjwa -Uzalishaji -Ukuaji Hii itakupa mwanga wa kupata kuku bora au kukupa picha halisi ya nini uwafanyie kuku wako Mara baada ya kuwapata na kabla ya kuchanganya na kuku wenyeji. 2: Unatakiwa kuandaa sehemu maalumu, au chumba maalumu kwaajili ya kupokelea hao kuku wageni na kuwatenga kwa muda kabla ya kuwachanganya na wenzao. Hii itakusaidia kupunguza uwezekano wa kuleta maambukizi moja kwa moja kutoka kwa kuku wageni kwenda kwa kuku wenyeji  FANYA YAFUATAYO 👉Wapokee kuku wako kwenye chumba maalumu 👉Wape antibiotic kuwatibu kama walikuja na vimelea wowote Tumia broad spectrum (OTC) 👉Baada ya wiki 1 wapewe chanjo ya muhimu zaidi hasa Newcastle 👉Zoezi la kuwatibu kuku kabla ya kuwachanganya lichukue angalau wiki 2 👉Changanya kuku wako wageni na kuku wenyeji( hatua ya mwisho) 👉Ukichanganya kuku ongeza vyombo vya maji na  chakula 3: Epuka kufanya zoezi la manunuzi ya kuku na kuchanganya na w...

CHAKULA MBADALA

UOTESHAJI WA MAJANI HYDROPONICS FODDER Hydroponics ni majani au mboga mboga zinazooteshwa kwa muda mfupi...hapa naongelea majani au nafaka za kulishia mifugo HATUA ZA KUFUATA Unachukua aina yoyote ya nafaka mfano. Mtama, mahindi au uwele Unaosha nafaka utakayo amua kutumia kwa jiki kama inapatikana Baada ya hapoo unayatoa kwenye maji uliyokuwa unasafisha hizoo nafaka Unaloweka nafaka uliyoisafisha kwa maji safi kwa muda wa masaa 12 Baada ya masaa 12 nafaka yako itakuwa imeshapata maji ya kutosha Unaziweka nafaka zako kwenye chombo ambacho kinapatikana sana sana wanatumia trey maalum za kuwekea ambazo zipo kama sahani au sinia unazifunika kwa nylon yoyote lakini sana sana wengi wanatumia gazeti au nylon nyeusi Unaziweka kwenye chumba ambacho hakipitishi mwanga kwa muda wa masaa 48 Baada ya masaa 48 ukienda kufunua utakuta nafaka uliyochagua imeota nyuzi nyuzi nyeupe utatakiwa utoe trey za hiyo nafaka uliyochagua na kuweka sehemu iliyotengenezwa rasmi kama kichanja  tray zina beba gr...

MAGONJWA YA KUKU -MDONDO/KIDERI (NEWCASTLE DISEASE)

Ni ugonjwa unaowapata jamii ya ndege ambao unasababishwa na vimelea aina ya  paramyxovirus. Kuenea kwa Ugonjwa Ugonjwa wa Mdondo (Newcastle disease) huenea kupitia njia mbalimbali kama zifuatazo:- Mayai ya kuku aliyeugua ugonjwa wa mdondo/kideri (Newcastle disease). Kugusana na kuku mgonjwa. Kupitia maji yenye maambukizi. Wakati wa totoleshaji vifaranga. Chakula chenye maambukizi. Hewa yenye maambukizi ya ugonjwa huu. Dalili za Mdondo/Kideri (Newcastle disease) Vifo vya ghafla. 2. Kutoa udenda mdomoni. 3. Kukosa hamu ya kula. 4. Kuharisha kinyesi cheupe na kijani. 5. Kuhema kwa shida. 6. Kukakamaa viungo au kupooza hasa mabawa, shingo na miguu. 7. Kupunguza utagaji. 8. Vifo hutegemea kasi ya ugonjwa huweza kufikia hadi asilimia mia moja (100%). Namna ya kudhibiti Mdondo/Kideri (Newcastle disease) Wapewe chanjo kwa muda unaofaa (Siku ya 7 na 28, na kila baada ya miezi 3). Kuku wote waliozidiwa (wagonjwa) wachinjwe na wafukiwe katika shimo lenye kina kirefu kuzuia kuenea ugonjwa. Fua...

AINA ZA VYAKULA VYA KUKU

SOMO KUHUSU CHAKULA CHA KUKU. MASH: Chakula cha vumbi vumbi PELLETS: Chakula cha tambi tambi Kama ilivyo zoeleka kwa aina nyingine za mifugo, kuku pia wanatakiwa kupewa chakula sahihi katika umri sahihi ili kuwawezesha kukua vizuri na pia kutaga mayai vizuri. Makundi ya vyakula vya kuku( yaliyo zoweleka na wafugaji wengi ) Kwaajili ya kutaga(Layers breed, chotara na kienyeji 1: Super Starter/ Starter mash 2: Grower mash 3: Layers mash  UFAFANUZI Starter mash au Super starter mash, hiki ni chakula mahususi kabisa kwaajili ya vifaranga au kuku wanaoandaliwa kwaajili ya kutaga, chakula hiki hutakiwa kuwa na kiwango cha zaidi cha protini ili kuimarisha kinga za mwili wa kuku, pia wanga kusaidia ukuaji sahihi. Kwa kutegemea miongozo utakayo pewa, Chick starter au Layer starter inatakiwa kulishwa kwa kuku kuanzia wakiwa na umri wa siku 1 mpaka wiki ya 6 , 7 au 8 kwa kutegemea mwongozo wa Formula au kiwanda utakacho nunua Chakula. Starter inashauriwa kuku wapewe bila kipimo angalau kwa wi...

KUKU WA ASILI

KANUNI BORA ZA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI SOMAMPAKA MWISHO UJIFUNZE Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi. Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi. Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya; 1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni. 2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa. 3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa. ...